Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naipongeza sana Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuleta mapendekezo ya Mpango na Mwongozo wa kuandaa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizi kwa ufupi naomba nijazie vitu vichache ama niungane na wachangiaji wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee Mfuko wa Taifa wa Watu Wenye Ulemavu. Mfuko huu ni halali maana uliundwa kisheria ili kukidhi mahitaji mbalimbali ya watu wenye ulemavu ikiwemo suala la elimu na kadhalika. Naiomba Serikali katika mwaka wa fedha 2017/2018 mfuko huu utengenezwe na kupelekewa fedha za kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ruzuku za vyama vyenye watu wenye ulemavu, naomba vyama hivi vipewe ama vipelekewe ruzuku kama ilivyokuwa zamani ama miaka ya nyuma. Vyama vya watu wenye ulemavu vinashindwa kujiendesha na vingine vinaelekea kufa kabisa maana vimekosa fedha za kuviendesha. Naomba sana Serikali yangu ya CCM iliangalie tena na tena suala la ruzuku na Mfuko wa Taifa wa Watu Wenye Ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kifungu maalum kupitia Bunge, Sera, Ajira, Kazi na Walemavu; naiomba Serikali iweke kifungu maalum na kifungu hicho kipewe fedha kwa ajili ya mahitaji mbalimbali ya watu wenye ulemavu. Watu wenye ulemavu wana mahitaji mengi ikiwemo mafuta maalum kwa watu wenye ualbino, baiskeli za miguu mitatu au miwili, fimbo nyeupe, vifaa vya kuongeza usikivu (hearing aids) na kadhalika. Uwepo wa kifungu hicho chenye fedha, utasaidia mahitaji tajwa hapo juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, matengenezo ama ukarabati wa shule maalum, vitengo na shule zote za awali, msingi, sekondari na vyuo ili zifae kwa watoto ama wanafunzi wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vifaa vya kufundishia na kufundishiwa (teaching and learning aids), kuna uhaba mkubwa wa vifaa hivi kwa wanafunzi wenye ulemavu. Naiomba Serikali itoe kipaumbee kwa upatikanaji wa vifaa hivi ili WWU (Watu Wenye Ulemavu) waweze kupata elimu ambayo ndiyo mkombozi wa maisha yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkalimani wa lugha ni chakula kwa mlemavu; kiziwi, hivyo naiomba Serikali katika mwaka wa fedha 2017/2018 itengwe bajeti na waajiriwe wakalimani hawa (kwenye Televisheni ya Taifa, Hospitali za Serikali, Viwanja vya Ndege, Vituo vya Polisi na kadhalika); kwa vyombo binafsi kama televisheni, hospitali na kadhalika. Serikali itoe tamko la kuviamuru vyombo hivi viajiri wakalimani hawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haya machache, naomba kuwasilisha.