Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo mengine naleta mapendekezo ya masuala kadhaa yakiwemo na ya kwenye Mpango wa Serikali wa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, Uanzishwaji wa Mkoa Mpya wa Ulanga kama RCC ya Mkoa wa Morogoro ilivyoridhia kuanzishwa kwa Mkoa wa Ulanga wenye Wilaya tatu, Kilombero, Ulanga, Malinyi. Pia napendekeza mpango uweze kupendekeza kuanzishwa Wilaya ya Mlimba ambapo utakapotangazwa Mkoa wa Ulanga uwe na Wilaya nne; Ulanga, Malinyi, Kilombero na Mlimba ili kusogeza huduma kwa wananchi. Pia mpango uoneshe kuwepo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba ambapo mchakato wa upatikanaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba umeshakubaliwa na Baraza la Madiwani la Kilombero na hatua zinaendelea kufanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza mpango ueleze ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya Ifakara hadi Mlimba kilomita 153, pia Mlimba – Madeke – Njombe kuunganisha mikoa hiyo miwili. Umuhimu wa barabara hiyo unatokana na kupatikana kwa kilimo cha mpunga na shamba la uwekezaji la KPL Mngeta. Pia mradi mkubwa wa umwagiliaji wa Njage, kilimo cha miwa Ruipa na ujenzi wa kiwanda cha sukari, upatikanaji wa mazao ya biashara kama cocoa, ufuta, ndizi, matikiti na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia umuhimu wa barabara hiyo ni kumrahisishia mwananchi kusafirisha mazao, kwenda kufuata huduma za matibabu hasa kwa mama mjamzito na mtoto kwani hospitali ya Wilaya iko umbali wa kilomita 263 hivi na barabara haipitiki kipindi chote cha mwaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango uingize upatikanaji wa maji katika Mji wa Mlimba ambapo Serikali ione umuhimu wa kusambaza maji yanayopatikana kwenye mito mikubwa iliyoko Mlimba kama vile Mto Mpanga na Mnyela baada ya kuchimba visima ambavyo vingi havina maji ya kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango uweke ujenzi wa vituo vya afya kila Kata na hospitali ya Wilaya Mlimba. Pia ujenzi wa kituo cha Polisi Mlimba na Mahakama za Mwanzo katika Kata 16 za Jimbo la Mlimba. Vile vile Mpango uzingatie ajira za Walimu, watumishi wa afya hasa vijijini. Ahsante.