Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Umaskini na Athari Zake; kukithiri kwa umaskini kunazalisha uhalifu na ndio unaoondoa amani katika Taifa. Hivyo basi nashauri hatua za kuondoa umaskini zifanye jitihada za haraka ili kunusuru nchi na majanga ya uvunjifu wa amani kunakopelekea magereza kujaa wahalifu na kupelekea Taifa kubeba mzigo mkubwa wa kuwatunza wafungwa badala ya kuelekeza fedha hizo kwenye maendeleo ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ongezeko la Watu. Ifikapo 2020/2026 idadi ya watu itafikia milioni 63 ambayo kama utekelezaji wa mpango wa miaka mitano hauwiani na ongezeko hilo italeta shida kwenye huduma za jamii wakati huo, hivyo ndoa za utotoni zithibitiwe kupunguza ongezeko.
Mheshimiwa Naibu Spika, Elimu. Bila elimu yenye tija Taifa haliwezi kufika kwenye uchumi wa kati. Elimu yetu haisaidii kijana kujiajiri, ni vyema kila Mkoa kukawa na scheme for irrigation ili kumeza ombwe kubwa la vijana wanaomaliza shule ili kuwafanya wasigeuke kuwa wahalifu katika Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, madhara ya ukosefu wa ajira kwa vijana kunasababisha uhalifu kuongezeka hivyo kusababisha ongezeko la ajira za Polisi na Magereza na hivyo kuongezeka kwa matumizi kwa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kukosa ajira kunasababisha utumiaji madawa ya kulevya hivyo kuligharimu Taifa kuwatibu kwa gharama kubwa na pia kutokana na hali ngumu ya maisha na utumiaji madawa ya kulevya, UKIMWI umeanza kushika kasi sehemu nyingi katika nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama Taifa tuangalie nguvukazi ya Tanzania ambayo iko asilimia 60 ya wananchi wa Tanzania kuwa mzigo kwa nchi, hivyo Taifa lijipange kunusuru tatizo hili ambalo miaka ijayo Taifa halitaweza kulimudu, hilo ni kundi la vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kilimo ni uti wa mgongo, naomba iainishwe vijana wametengewa ekari ngapi ili waweze kujiajiri, pia njia ambazo Taifa litawawezesha.