Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira ilikutana na wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara wakubwa wanaotumia Bandari ya Dar es Salaam ambapo walieleza kwamba mizigo imepungua kwa kiasi cha asilimia 42 na mingi ni ile inayopita kwenda nje ya nchi hususan Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maelezo ya wadau kupungua kwa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam kumesababishwa na kutozwa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa huduma zinazotolewa katika mizigo au bidhaa inayopitia bandari hiyo kwenda nchi jirani (VAT on auxiliary services on transit goods) za Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Zambia, Malawi, Burundi, Rwanda na Uganda. Kutozwa Kodi ya Ongezeko la Thamani katika tozo mbalimbali za bandari kunaongeza gharama ya huduma na biashara katika Bandari ya Dar es Salaam na kupunguza ushindani na bandari nyingine kama zile za Nacala, Beira, Mombasa na Durban. Hivyo basi, ili tuweze kufikia uchumi wa kati, ifikapo mwaka 2025 ni lazima tuiangalie bandari yetu na pia tupunguze ushuru ili tuweze kuzalisha mapato mengi katika Taifa letu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.