Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, single customer territory imeanza utekelezaji wake mwaka 2014 Januari, kwa nchi za Kenya na Uganda na kwa Tanzania imeanza rasmi Julai, 2014. Changamoto mpaka sasa kwenye himaya hii ya forodha ya pamoja ni kwamba kati ya nchi zote tano za Afrika Mashariki ni Tanzania na Rwanda pekee ambazo zinatekeleza makubaliano haya kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Uganda na Kenya bado wanakusanya kwenye baadhi ya bidhaa tu, huku Burundi ikiwa haijawahi kutekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, dhana hii ya SCT ni njema sana kama itakuwa inatekelezwa na nchi zote wanachama. Ndio maana nchi ya Congo DRC imeomba iingizwe katika utaratibu huo. Ni jukumu la Serikali kuhakikisha kuwa nchi zote zilizoridhia SCT zinatekeleza ili kudhibiti unyonyaji wa mapato kutoka kwa baadhi ya nchi ambazo hazitekelezi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali yetu iwasiliane na Serikali ya Jamhuri ya Mozambique ili kupitia bandari ya Beira pia utaratibu huu uweze kutumika. Hii itasaidia kuwadhibiti wale wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu.
Mheshimiwa Naibu Spika, faida za SCT; kudhibiti ukwepaji kodi kupitia mizigo ya transit, hapo awali kabla ya utaratibu huu mizigo mingine ilikuwa inashushwa ndani ya nchi yetu, hivyo kuwepo na ukwepaji kodi na kuikosesha Serikali mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushindani hafifu wa kibiashara, kwa sababu wafanyabiashara hasa wakubwa walikuwa favored na utaratibu huo, kuliko wajasiriamali wadogo. Wasafirishaji wa mizigo kwenda Congo wamekuwa wakifanya trip nyingi zaidi baada ya utaratibu huu wa SCT kwa kuwa hakuna usumbufu, tofauti na ilivyokuwa huko nyuma; ilikuwa inawagharimu wasafirishaji zaidi ya miezi miwili hadi minne kusafirisha na ku-clear mizigo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo; ufufuaji wa zao la Mkonge katika Mikoa ya Tanga, Morogoro na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani, zao la mkonge limepanda thamani sana duniani na kati ya mashamba 56 yaliyopo nchini mashamba 37 yapo Mkoa wa Tanga na mengi yamekuwa mapori.
Mheshimiwa Naibu Spika, Bandari, Bandari ya Tanga ifufuliwe na kupanuliwa ili iende sambamba na ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda–Ziwa Albert hadi katika Bandari ya Tanga. Hii itasaidia pia usafirishaji wa mizigo kutoka Tanga Tanzania hadi Uganda na nchi jirani ya Sudani Kusini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Viwanda, Kiwanda cha Afritex kilichokuwa kina uwezo wa kuajiri wafanyakazi 2000, kimefungwa na kipo Mkoani Tanga kikitengeneza aina mbalimbali za bidhaa za nguo. Serikali inakosa mapato, lakini pia ajira inapungua kwa kiasi kikubwa. Ahsante.