Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kumteua Waziri wa Fedha ambaye anajua vizuri uchumi wa nchi; nampongeza Naibu Waziri kwa utendaji mzuri, napongeza juhudi za Serikali kwa kutuletea Mpango mzuri wa Maendeleo 2016/2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango nitachangia ukurasa 13, Ujenzi wa Barabara ya Mwendokasi katika Jiji la Dar es Salaam. Naomba Serikali iboreshe mpango wake wa kuendesha mabasi yaendayo kasi kwani usafiri huo ni bora sana na ni msaada mkubwa sana kwa wananchi wetu. Sasa mradi wa mabasi yaendayo kasi yaelekee phase II kutoka Kariakoo kwenda Mbagala.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukamilishaji wa Kituo cha Biashara cha Kurasini. Kituo hiki ni muhimu sana na Serikali sasa imekamilisha malipo ya fidia na kuanza utaratibu wa ujenzi wa ukuta.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema kituo hicho kikaendelea kuwepo na kifanye kazi kwa maslahi ya Watanzania na wale wengine wageni wanaotoka nchi za jirani kuja kununua bidhaa zao Kurasini, lakini pia, Kurasini kutakuwa ni mji mzuri wenye maendeleo na mvuto mkubwa wa kibiashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa flyover TAZARA- Serikali iendelee na mpango wake wa ujenzi wa barabara za juu kwa eneo la TAZARA ni jambo la maana sana. Katika kupunguza msongamano katika barabara zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iongeze mtaji Benki ya TIB ili iongezee uwezo wa kukopesha wafanyabirashara, wajasiriamali kwa kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo viwanda badala ya kutumia Mifuko yetu ya Pensheni katika maeneo mengi ya viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo, Mpango uelekeze kwenye kukiendeleza kilimo cha mazao ya chakula na biashara. Pembejeo za kilimo ziwafikie wakulima kwa wakati. Wananchi waweze kuboresha kilimo na kupata mazao mengi ya chakula na biashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha standard gauge; ni vyema reli iwepo kwa kuwa itatusaidia sana katika kukuza uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa viwanda ni vyema kabla hatujajenga vipya kwanza tuangalie vile viwanda vya zamani. Tuangalie ni nini kilitufanya tuanguke na tuvifufue angalau vichache, pia viwanda vipya vianzishwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Mheshimiwa Waziri kaza buti, Hapa Kazi Tu.