Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kabla sijachangia mpango huu wa Serikali naunga mkono hoja. Nimpongeze Waziri wa Fedha na Naibu wake pamoja na watumishi wote wa Wizara ya fedha walioshiriki katika kuandaa mpango huu ambao unalenga katika kuinua uchumi wa Taifa letu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimepitia mpango huu mambo mengi yaliyomo ndani mpango huu yana nia ya kuinua uchumi wa nchi yote kwa leo. Nitajikita kwenye maeneo machache ambayo yanahitaji usimamizi na mkakati wa hali ya juu. Maeneo hayo ni Sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji, Sekta ya Utalii pamoja na kutazama upya aina ya kodi mbalimbali zinazotozwa na Mamlaka ya Mapato (TRA) hususan kwa wafanyabiashara wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Kilimo ni muhimu sana ikisimamiwa kwa karibu na kwa njia za kisasa ni eneo ambalo kwa kiasi kikubwa itachangia pato la Taifa letu. Eneo ninalosisitiza hapa ni kilimo cha umwagiliaji, nchi yetu imebahatika kuwa na ardhi nzuri yenye rutuba, pia na mabonde mengi. Je, Serikali haioni umefika muda badala ya kutegemea kilimo tulichozoea cha kutegemea mvua, tutumie fursa za mabonde yetu kuzalisha mazao mbalimbali ya chakula na biashara. Aidha, kupitia mpango huu tunaweza kuchimba mabwawa makubwa pamoja na visima virefu ili kilimo chetu kisitegemee mvua tu. Ni muhimu sana kwani ni Mataifa mengi yameweza kupiga hatua, aidha tatizo la vifaa la kila wakati litatuliwa
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine ambalo ningependa Waziri wa Fedha alitazame katika kuinua pato la nchi yetu ni Sekta ya Utalii. Nchi yetu ina maeneo mengi ya utalii kwa maana mbuga mbalimbali za utalii, lakini bado sekta hii inachangia kiasi kidogo si kwa kiwango ambacho kama Wizara husika ingekuwa na mkakati na mpango thabiti, Taifa lingefaidika sana. Bado naamini hatujaweza kutangaza sekta hii ipasavyo, aidha, gharama au tozo tulizoweka katika utalii zimepunguza ujio wa watalii ni vema tukubaliane wenzetu wa nchi jirani nao wana fursa kama yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mbuga zetu zina wanyama wengi, hivyo tuweke mkazo katika eneo hili, niipongeze Serikali kwa kununua ndege mpya nikiamini zitasaidia ujio wa watalii ambao awali walikuwa wakifikia nchi jirani. Niiombe Serikali yetu pia iboreshe huduma katika mahoteli ambapo watalii wanafikia, pia kodi kwa watalii ipunguzwe kwani imepunguza idadi ya watalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ningependa kutoa mchango juu ya kodi mbalimbali zinatozwa na Mamlaka ya Mapato (TRA), nchi yoyote duniani haiwezi kusonga mbele bila ya kodi; mipango yote ya maendeleo inategemea kodi hata nchi yetu bila ya kodi haiwezi kusonga mbele. Naunga mkono suala la kodi ila nina mawazo tofauti juu ya utitiri wa kodi na juu ya ukadiriaji wa kodi, eneo hili lina matatizo kwani ukadiriaji huu hauna uhalisia, aidha watumishi wote wa TRA wanakosa njia iliyo sahihi ya ukadiriaji kwani wananchi wengi wamekuwa wakilalamika sana kukadiriwa kiwango kikubwa ambacho hakilingani na uhalisia wa biashara zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali ione njia nzuri ya kupitia TRA ili ipunguze malalamiko haya. Wananchi wengi wana nia ya kulipa kodi, tusiwakatishe tamaa wananchi wote nikiamini kabisa bila kodi hakuna uhai. Ni imani yangu Mheshimiwa Waziri na Serikali watayapokea maoni haya.