Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ALI HASSAN KING: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu definition (maelezo), recognition na money measurement kwa item ambayo imo katika Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, Definition Maelezo (Broad or Narrow definition), naishauri Serikali kuwa maelezo au definition ya item ambayo imo ndani ya mpango wa maendeleo wa Taifa iwe inahusiana na sehemu ya jambo ambalo litatekelezwa kwa kipindi hicho kuliko kueleza mradi wote ambao unatekelezwa kwa muda wa miaka mingi ijayo. Mfano, mradi wa Mchuchuma na Liganga, katika miradi hii imeelezwa kwamba itaanza na kumalizika ndani ya muda huo huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, recognition, napendekeza kuwa item ambayo itaingizwa humu kama ni mpango iwe imetimiza kigezo ambacho hatua za utekelezaji zitakuwa karibu na utekelezaji ikiwemo mikataba na muda wa dhamira ya kutekeleza ndani ya muda uliowekwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, measurement, fedha zitakazotajwa kutekeleza jambo hilo ziwe zimezingatia muda wa utekelezaji shughuli zilizoainishwa kutekelezwa na kadhalika. Kwa mfano, miradi ya Mchuchuma na Liganga imepangwa kutumia kwa jumla ya dola za Kimarekani bilioni mbili nukta tisa ambazo takribani ni shilingi trilioni sita za Kitanzania wakati katika kugharamia mpango sekta binafsi inakadiriwa kuchangia kwa shilingi trilioni saba nukta nne za Kitanzania. Miradi ya Mchuchuma na Liganga ni mfano tu lakini kwa maeneo mengi kama vile uanzishwaji wa kituo cha biashara Kurasini, ujenzi wa reli ya kati.
Mheshimiwa Naibu Spika, wingi wa fedha za maendeleo na ukuaji wa mapato ya ndani. Fedha za maendeleo kwa mwaka 2015/2016 zilikuwa trilioni nne nukta tatu, fedha za maendeleo kwa mwaka 2016/2017 zilikuwa trilioni 11.820 lakini ongezeko la makusanyo ya ndani yanakuwa kidogo. Tumeongeza fedha za maendeleo ili tuongeze uwezo wa mapato ya ndani ili tupunguze kukopa, lakini mikopo nayo inaongezeka badala ya kupungua.
Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kuangalia kuwa fedha za maendeleo kwanza zilenge kwenye miradi itakayotoa majibu kwa haraka ili ichangie katika kukuza mapato ya ndani.