Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-
(1) Mdororo wa uchumi umesababishwa na sera za uchumi wetu. Wakati Serikali imetumia sera zote mbili za fiscal policy kubana matumizi na kuongeza kodi katika bidhaa na huduma mbalimbali. Benki Kuu imekaa kimya kabisa bila kuchukua hatua zozote katika kupunguza riba za mabenki na kusimamia mzunguko wa fedha nchini. Hali hii ndiyo iliyosababisha mabenki kuporomoka na kushuka kwa uchumi. Fedha zimepungua kwenye mzunguko.
(2) Kupungua kwa uzalishaji bidhaa na kushuka kwa ajira nchini. Hivi sasa viwanda na makampuni mengi yameanza kupunguza wafanyakazi kama kwenye sekta ya utalii, hoteli na taasisi za elimu.
(3) Lazima Serikali ianze kurasimisha Sekta binafsi na kuziunga mkono ili zichangie katika pato la Taifa.
(4) Kuhamasisha kilimo kikubwa cha mazao ya chakula na biashara kwa kutoa support inayohitajika pamoja na masoko ya bidhaa.
(5) Kuendelea kuhakikisha kuwa Serikali inahamasisha na kusimamia sera ya elimu ikiwa ni pamoja na kuanzisha mitaala yetu ili iendane na mahitaji ya soko na kuongeza udahili ili nchi iwe ya wasomi wengi.
(6) Kuangalia vipaumbele ambavyo vina competitive advantages kufuatana na mazingira na jiografia ya nchi yetu. Lazima uchambuzi wa kina ufanyike. Kwa mfano; Bahari, Bandari, Mlima Kilimanjaro, Mbuga za Wanyama, Madini, Olduvai Gorge na kadhalika.
(7) Kuimarisha matumizi ya reli ya TAZARA ili kupunguza gharama za uzalishaji na uharibifu wa barabara katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ikiwa ni pamoja na kupambana na rushwa, ubabaishaji na kadhalika.