Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya Bunge ni kuishauri na kuisimamia Serikali ili kuongeza ufanisi. Wabunge kwa nyakati mbalimbali wanashauri, ni vizuri Serikali ikawa sikivu na kuchukua ushauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bunge la Bajeti, Wabunge walipigia sana kelele masuala ya VAT kwenye utalii; VAT on transit, single customs territory kuunganisha RAHCO na TRL na kadhalika. Nchi imeendelea kupoteza mapato ya mabilioni ya fedha na hakuna hatua zinachukuliwa, kama nchi sasa tumekuwa mawakala wa kukusanya kodi kwa nchi ya DRC.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo kinaajiri zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania, uwekezaji kwenye sekta ya kilimo haukwepeki ikiwa kweli tumeamua kuwa nchi ya viwanda na uchumi wa kati. Mpango utoe kipaumbele kwa agro-processing industries. Watanzania asilimia 80 wasiwe watazamaji tu katika mpango huu bali wawe ni sehemu muhimu ya mpango huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo chetu kimekuwa tegemezi kwa mvua ambazo hazitoshelezi. Ni muhimu sana tufanye mapinduzi katika kilimo ili kilimo cha umwagiliaji wa kutumia mabwawa na visima virefu kipewe kipaumbele. Pia, masoko ya mazao hayana uhakika, msimu wa 2015/2016 kilogramu moja ya Mbaazi ilikuwa sh. 3,000 na msimu huu wa 2016/2017 bei ya kilogramu moja ni sh. 800. Wakulima wa Mbaazi wamekata tamaa kabisa, ruzuku ya kilimo haipatikani kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo Benki ya Kilimo ambayo iko Dar es Salaam, benki hii iongezewe mtaji na ikopeshe wakulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya huduma za afya nchini ni mbaya sana, hakuna dawa kwenye vituo vya afya, hakuna vifaatiba na pia watalaam hawatoshi, ni vema mpango huu uhakikishe hospitali za Wilaya, vituo vya afya na dispensary vinatoa huduma stahiki kwa wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu katika kuleta mageuzi ya uchumi wa viwanda nchini.