Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono jitihada zinazofanyika katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo wa 2016/2017 hadi 2020/2021, mkakati ni mzuri uelekeo unatoa picha kubwa ya matumaini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya kwanza, Utekelezaji wa Miradi ya Kipaumbele kama Taifa; Ushauri, miradi ya kielelezo itekelezwe kwa umakini kama Taifa, we need action and not words. Miradi ya Reli ya Kati, Kanda Maalum za Kiuchumi, Bagamoyo, Kigoma, Mtwara na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Bandari ya Kidahwe-Nyakanazi na Manyovu, Kasulu; miradi hii ni muhimu sana itekelezwe hata kama ni kukopa fedha kutoka nje au ndani, imepangwa vizuri itekelezwe kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya pili, ukurasa wa 28; Hotuba ya Mheshimiwa Waziri, Kikosi Kazi cha Maboresho ya Kodi kiangalie vyanzo vipya vya mapato (New Tax Revenues) mfano, angalieni Economic za Uvuvi wa Bahari Kuu, tunaambiwa ni eneo lenye kuweza kuchangia pato kubwa la Taifa hili. Uzoefu wa nchi za Singapore, Thailand na Austria unatoa rejea sahihi kabisa. Tuwekeze huko, tununue meli ya uvuvi na tuboreshe gati namba Sita, ambayo imetolewa na Mamlaka ya Bandari (TPA), kama bandari yetu kituo cha kupokea mavuno hayo ya Bahari Kuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Taasisi za Umma ambazo Serikali inamiliki hisa zake ukurasa wa 43 hadi 44 wa hotuba ya Waziri; taasisi za Tipper, PUMA Energy, Kilombero Sugar ni taasisi ambazo Serikali yetu ina hisa, lazima tuwekeze huko. Taasisi za Tipper na PUMA Energy ambako Serikali ina asilimia 50 ni maeneo ambayo yakisimamiwa vema na Serikali kuweka nguvu yanaweza kuongeza pato la Taifa letu. Kampuni hizo zipewe support ili zizalishe mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushiriki wa sekta binafsi kupitia PPP; Mheshimiwa Waziri, dhana hii inafahamika vizuri Serikalini? Ipo wapi miradi ya PPP mfano, ujenzi wa barabara ya Chalinze- Dar es Salaam wako wapi sekta binafsi? Ushiriki mdogo wa sekta binafsi kutokana na Mazingira yasiyowezeshi ya uwekezaji, angalieni upya vikwazo vinavyokwamisha ushiriki wa private sector, tatizo lazima libainishwe na lipatiwe dawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukurasa wa 40 kupitia upya ada, ushuru na tozo ili kuzirekebisha ziendane na maendeleo na ustawi wa jamii. Kikosi kazi kiangalie tozo kwenye pamba, kahawa, tumbaku, mkonge, chai na kadhalika ili mazao haya yalimwe kwa tija bora zaidi kuliko ilivyo sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii.