Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kushauri Serikali kwenye Mpango wa mwaka 2017/2018 kama ifuatavyo:-
(i) Kilimo; kuongeza nguvu kubwa ya kuwasaidia wakulima kwa kuongeza pembejeo za kilimo na mbegu yenye ruzuku, kwa mikoa inayozalisha mazao mengi ya chakula na biashara.
(ii) Mifugo; ni muhimu kupunguza ama kuondoa kabisa migogoro ya wafugaji na wakulima, kwa kuwatengea maeneo maalum kwa ajili ya malisho ya mifugo yao.
(iii) Elimu; ni muhimu kwa Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kuanza mean test mapema kwa ajili ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu wanaoomba mikopo, ili kupunguza matatizo yanayotokana na kukopeshwa kwa wahitaji hao. Elimu ya shule zetu iwe ni kwa vitendo zaidi kuliko nadharia.
(iv) Afya; ni muhimu kupanga bajeti ya afya ambayo itakuwa inalenga kujitegemea kama nchi kuliko kutegemea wafadhili. Mfano, magonjwa kama ya UKIMWI, dawa zake zinategemea zaidi Global fund na President‟s Emergency Plan for Aids and relief from America (PEPFAR) ambapo Serikali bajeti yake ni kidogo sana na hivyo inaweza kupelekea maafa makubwa kama wafadhili hawa watajitoa na ukizingatia kuwa sera za nchi zao zinabadilika.
(v) Telemedicine; ni muhimu Wizara ya Afya kufanya matibabu kwa njia za mtandao yaani telemedicine.
(vi) Barabara (Miundombinu); kuna umuhimu mkubwa wa kujenga barabara ya kutoka Katumba-Lwangwa –Mbambo-Tukuyu iliyopo Mkoani Mbeya Wilayani Rungwe. Barabara hii inatakiwa kujengwa kwa kiwango cha lami ili wananchi wa Majimbo yote matatu yaani; Busokelo, Kyela na Rungwe wanufaike kwa kuweza kusafirisha mazao mbalimbali kama ndizi, mpunga, kokoa, viazi mviringo, chai, mbao, mahindi na mazao mengine mengi, lakini pia usafirishaji wa gesi asilia aina ya carbondioxide (Co2).
(vii) Geothermal (Nishati ya Umeme); ni muhimu kama nchi kuweza kuanza kuwekeza kwenye umeme wa joto-ardhi ambao unapatikana Jimbo la Busokelo, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya eneo la Kata ya Ntaba.
Mheshimiwa Naibu Spika, nategemea mapendekezo yangu yatapewa kipaumbele.