Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa hizi dakika tano japo ni chache sana nitajitahidi kwenda katika point form. Kwanza kabisa niseme kwamba naunga mkono taarifa zote mbili za Kamati ya PAC na LAAC. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kikubwa nichangie kwanza kabisa kwenye misamaha ya kodi. Tumekuwa tukiongea kama Bunge na kuishauri Serikali kwamba walau misamaha ya kodi iwe angalau chini ya asilimia moja ya Pato la Taifa. Ukisoma taarifa ya PAC utaona kabisa wameainisha misamaha ya kodi isiyokuwa na tija kwenye Taifa letu na mbaya zaidi inatolewa kwenye makampuni mengine ambayo hayana leseni, mengine wanasema yameghushi. Sasa swali hapa ambalo tungetaka tujue hawa watu ambao wamepewa hizi fedha, Serikali imechukua hatua gani, wameshazirudisha na kwa wale watendaji ambao waliidhinisha hii misamaha ya kodi ilhali watu wameghushi nyaraka, leseni zime-expire na mambo mengine wamechukuliwa hatua gani? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kingine ni suala zima la madeni ya Serikali kwenye Mifuko ya Hifadhi za Jamii. Siku Mheshimiwa Rais anaongea na wanahabari alisema kabisa kwamba mifuko hii inafilisika kikubwa ni kwa sababu wanasiasa na mbaya zaidi akasema Wabunge sisi ndiyo tunafilisi mifuko hii kwa sababu tumekopa. Kwenye ripoti hii ya PAC imeanisha kabisa zaidi ya shilingi trilioni 1.5 Serikali inadaiwa na Mifuko hii ya Hifadhi ya Jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi tunavyoongea kuna wafanyakazi fedha zao hazijapelekwa kwenye mifuko husika, kwa mfano, Askari Magereza na Polisi na wafanyakazi wengine tangu mwezi wa nne mpaka sasa hivi makato yao hayajaenda kwenye mifuko husika. Sasa tunauliza ni kwa nini Hazina wasipeleke hizi fedha za michango kwenye mifuko husika? Yaani mnakopa kwenye michango ya wafanyakazi bado mnakopa kwenye uwekezaji halafu Rais anauambia umma kwamba Wabunge ndiyo wamefilisi mifuko ya jamii, is he serious? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kingine, tumekuwa tukilalamika kuhusu kukaimishwa kwa watendaji kwenye mashirika ya umma lakini pia imekithiri kwenye Halmashauri zetu. Ni wakati sasa Serikali ione umuhimu wa either kuwajiri watu wenye uwezo kwenye vitengo mbalimbali, kwa mfano kwenye Halmashauri yangu ya Mji wa Tarime mara nyingi nimekuwa nikimfuata Waziri husika, kuna watendaaji wanakaimu kule, ufanisi ni zero, Halmashauri inakuwa haiwezi ikafanya vizuri. Naomba kabisa Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI ufanye juhudi na wale wengine ambao wanasimamia mashirika mbalimbali tusiwe tunakaimisha hizi nafasi inapunguza ufanisi wa kufanya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia 20 za ruzuku ambazo zinatakiwa kwenda kwa Serikali za Mitaa na Vijiji. Tumekuwa hata tukiuliza maswali humu ndani, wale Wenyeviti wa Mitaa hawalipwi posho, unakuta hata hawana stationary kwa hiyo wanashindwa hata kufanya kazi. Fedha ambazo mnapeleka kule kwenye Halmashauri haziwafikii Serikali za Mitaa au za Vijiji. Tunaomba sasa Wizara husika muweze kuwa na ufuatiliaji kama ni ripoti inakuwa inatolewa kuhakikisha kwamba hizi asilimia 20 kweli zinatengwa au hazitengwi na kama hazitengwi ni kwa nini zisiende kule chini na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine ambacho kinahuzunisha zaidi ni zile asilimia kumi kwa ajili ya vijana na wanawake. Kikubwa hapa kinakuja unakuta Halmashauri haina mapato, fedha wanazokusanya wanapeleka sehemu zingine. Kwa hiyo, hii ipo tu kwenye makaratasi kwamba wanawake wanapewa asilimia tano na vijana wanapewa vijana asilimia tano lakini kiuhalisia hakuna. Mfano kwenye Halmashauri yangu ya Mji wa Tarime hiyo kitu haipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo kubwa ni kwamba vyanzo vya mapato ni vichache, lakini kingine mnaelekeza kwamba fanya kitu fulani kwanza, kwa hiyo, priority ya kutoa fedha kwa ajili ya Mfuko huu kwa ajili ya vijana na wanawake haipo na hii inakuwa inayumbisha. Tunaomba sasa utiliwe mkazo kama nilivyopendekeza kwenye ruzuku ya asilimia 20 na kwenye hii ruzuku ya asilimia kumi ya vijana na wanawake napo Serikali kupitia Wizara husika wahakikishe wanawake na vijana wanaenda kunufaika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ambacho nilitaka nizungumzie…
NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Esther.