Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa hii. Nimshukuru Mungu sana kwa siku ya leo kufika, kwa sababu ni siku ambayo niliitarajia na niliitegemea sana. Nasema haya kwa sababu nimepata bahati ya kushiriki makongamano ya kitaalam ya jambo hili, mwaka 2013 kule Rwanda na mwaka 2014 kule Brussels, Ubelgiji.
Mheshimiwa Spika, kiufupi mkataba huu ni hovyo! kiufupi wenzetu hawana nia njema kupitia mkataba huu. Mkataba huu umejadiliwa kwa miaka 12, miaka 12 nchi zetu zimekuwa kwenye majadiliano ya mkataba huu and yet tuna mkataba mbovu kiasi hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, huu ni mkataba ambao nchi yetu imeamua kuchukua njia ya kidiplomasia kusema kwamba inajitoa kwa sababu Uingereza inajitoa kwenye European Union, kauli ya kidiplomasia, lakini nchi ya Tanzania tumeheshimika duniani kwa kusimamia tunachoamini, tusijifiche kwenye diplomasia hii, tuwaambie ukweli hawa wenzetu ambao hawana nia njema na sisi. Tuwaambie ukweli kwamba tunathamini Utanzania wetu, tuwaambie ukweli kwamba tunajiheshimu na hatuko tayari kupuuzwa kupitia mkataba huu.
Mheshimiwa Spika, mambo mengi yamesemwa, loss of revenue, kulinda viwanda vya kati na vidogo, yamesemwa kuhusu rendezvous clause, mimi nataka niya-sum up kwa mambo haya machache nitakayouliza.
Mheshimiwa Spika, wakati nikisoma mkataba huu najaribu kujiuliza hivi mkataba huu unakusudia kutuongezea uzalishaji katika nchi zetu? Jibu ni hapana. Hivi mkataba huu unatuhakikishia usalama wa chakula? Jibu ni hapana. Hivi mkataba huu unatuongezea fursa za ajira zenye staha katika nchi zetu? Jibu ni hapana. Hivi mkataba huu unatuwezesha kutoka katika uchumi wa kutegemea natural resources exportation na kwenda kwenye production of sophisticated products? Jibu ni hapana. Lakini kilichowazi ni mkataba wa kutweza utu wetu, tufike mahali tuwaambie mchana kweupe macho makavu, kwamba hatutakubali kudhalilishwa.
Mheshimiwa Spika, tuupinge mkataba huu. Nakushukuru sana.