Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi na mimi nichangie kwenye mada ya leo. Nilipokuwa ninausoma mkataba hisia zikanipeleka kwenye historia. Miaka takribani mia moja iliyopita na zaidi walikuja wazungu na mikataba, lakini kabla ya kuja wazungu na mikataba wazungu walisitisha biashara ya utumwa na katika tangazo la kusitisha biashara ya utumwa ukisoma verses zilizokuwemo mle ni pamoja na kusema kwamba hii nguvu kazi ambayo tulikuwa tunaichukua tunaisafirisha ibaki kulekule ili izalishe kwa ajili ya viwanda vyetu. Baada ya hapo walifungua mashamba makubwa, mashamba yale yalikuwa ni kwa ajili ya kuzalisha malighafi zilizokuwa zinahitajika kwenye viwanda na wakati ule ndiyo ilikuwa mapinduzi ya viwanda yanafanyika Ulaya. Kwa hiyo, dalili zote za mfanano wa mikataba ya wakati ule imo kwenye huu mkataba, kwa hiyo mkataba huu una harufu ya ukoloni. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, yamezungumzwa mengi na wenzangu na mimi nirejee kwamba hakuna mkataba mbovu ambao nimewahi kuushuhudia kama huu kuanzia mwanzo tu. Pale kwenye kurasa za mwanzo kabisa ukisoma jinsi nchi zetu zilivyoorodheshwa, zimeorodheshwa kama block moja kwa moja, lakini walivyokuja kuorodhesha nchi zao wakaorodhesha moja moja halafu baadaye wakasema and the EU, hii aliisema mwanzoni kabisa Mheshimiwa Lugola. Mimi kuanzia hapo tu nilipata wasiwasi na nikapata wasiwasi zaidi hata wataalam wetu ambao walikuwa wanakwenda ku-negotiate tangu miaka ile ya 2007 mpaka juzi, nilipata wasiwasi kama kweli walikuwa wanajiandaa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, viwango vilivyomo humu vya terms kwa asilimia zaidi ya 80 ni vya ukandamizaji, kutukandamiza sisi na mengine yamo humu yanalazimisha kwamba tukisaini mkataba huu ndiyo tutapata hata masuala ya development cooperation. Sasa suala hili limenisumbua sana kama ambavyo limewasumbua Wabunge wengine, ninaomba niunge mkono wale wote ambao wametoa wito, Serikali isikubali kusaini mkataba huu mpaka pale marekebisho makubwa yatakapokuwa yamefanyika ikiwemo kuruhusu nchi mojamoja kujitoa wakati wowote inapoona kuna hatari. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ningezungumza mengi lakini mengi yameshazungumwa itakuwa ni kurudia, ninaomba niishie hapo, wote tuunge mkono kukataa kukataa mkataba huu. Ahsante sana.