Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. In principle, nakubaliana na mawazo ya Serikali kwamba mkataba huu tusiusaini, lakini kuna mambo ambayo kama Wabunge na kama wawakilishi wa wananchi lazima tuyajadili kwa pamoja tuone faida na hasara. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, napingana sana na wenzangu wanaofika hapa wanasema kwa sababu Mheshimiwa Mkapa amesema, Mheshimiwa Magufuli amesema, kwa hiyo, hatuusaini.
Mheshimiwa Spika, wajibu wetu sisi kama Wabunge hapa na hii ndiyo tabia ya Watanzania wengi, hatupendi kuhoji, hatupendi kudadisi, hatupendi kubishiwa. Hiki kitu kimekuja hapa, tuna haki ya kuhoji, kudadisi na kuuliza ili tukubaliane. Sisi siyo nyumbu kwamba tuingie tu mtoni, kwa nini mnataka tusidadisi? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, huu mkataba wataalam walipokuja juzi hapa, Profesa Kabudi alifafanua vizuri sana, lakini katika article 140 na kitu, alizungumza article karibu 20 au 15. Alizijadili hapa vizuri sana kwa weledi. Sisi kama Taifa amezungumza vizuri sana dada yangu hapa, tuna tabia ya ku-complain, tuna tabia ya kulialia! Complainers attract complainers. Kila wakati tunalalamika. Nakubaliana kabisa kwamba hii ni vita. Kila mtu anataka kupata hii keki ya uchumi duniani; kwa nini mnadhani Kenya wakubaliane na sisi kama wao hawapati maslahi? Kwa nini mnafikiri Europeans waje hapa kufanya mikataba kama wao hawana maslahi?
Mheshimiwa Spika, ni wajibu wetu sisi kama Taifa kutengeneza mazingira ambayo na sisi tuta-capitalise kupata faida. Siyo kila saa tunakuja hapa tunalialia, Kenya wametuzidi, Kenya wametuzidi. Kama wewe ni mpumbavu, upumbavu wako hauwezi kutoka kwa sababu unamchukia mwenye akili. We are responsible kujifunza kwa nini Kenya kila siku wanakuwa pro-active na sisi tunachelewa ku-capitalise huko mbele? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, wenzetu tunalia nao hapa kwamba wana mazingira mazuri. Sisi hapa tunalalamika; Mzee wa sound hapa kila siku ana viwanda vya kwenye mabegi. Sasa kama tuna viwanda vya kwenye mabegi, tutaenda kuuza nini Ulaya? Kutokuwa na kitu cha kuuza Ulaya is that their problem or is our problem? Badala ya kwamba sisi tukae hapa tujadiliane ni kitu gani tutapeleka Ulaya, tunalaumu kwa sababu hatuna kitu cha kuuza Ulaya. Is that their fault? That is our fault. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tumezungumza kwenye bajeti iliyopita, tumelalamika sana jinsi ambavyo Wizara ya Mambo ya Nje, imekuwa dhaifu katika masuala ya diplomasia ya kiuchumi. Ni kwa sababu hatuna wataalamu ambao wanaangalia mbele kuangalia Tanzania tunahitaji nini.
Mheshimiwa Spika, amezungumza dada yangu hapa, ukianza kujiuliza kaka yangu Mwijage hivi tunahitaji nini? Kwenye East Africa tunataka kupata nini? Tunataka kufanya biashara ipi? Iko kwenye makaratasi hapa halafu mnataka kutuambia Waheshimiwa Wabunge tukienda kwa wananchi...
Taarifa...
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Nakushukuru kwa taarifa, lakini wazungu sio watawala wa Kenya. Kenya inatawaliwa na Uhuru Kenyatta ambaye ni Mswahili.
Mheshimiwa Spika, ninachotaka kusema hili suala la blame shift, kila siku tuna-blame wengine tunashindwa kuwa responsible kwa uchumi wetu, hebu tuliache. Kwa sababu Wizara ya Mambo ya Nje ina udhaifu mkubwa sana katika nchi hii katika masuala ya diplomasia ya kiuchumi.
Mhemiwa Spika, nimemuuliza ni kitu gani tunataka kama Taifa upande wa Afrika Mashariki, ni kitu gani tunataka SADEC? Tunakuja hapa tunalialia tu, lakini hatujui tunataka nini. Hebu tuambie kwa mfano Wabunge tunataka tufanye biashara vipi na Afrika Mashariki, Ulaya, Marekani, Afrika ya Kusini au na Brazil? Tunataka tufanye biashara gani? Tunayo mikataba.
Mheshimiwa Spika, la pili, tumezungumza juzi kwenye ripoti ya …
Mheshimiwa Spika, naomba unilinde kwenye muda wangu, naona wanani-disturb sana.
Mheshimiwa Spika, kwenye ripoti ya GCI imezungumza sana jinsi ambavyo mazingira hata ya kufanya biashara katika nchi yetu ni magumu sana; mojawapo ya mazingira magumu ni kwamba Tanzania hatuna utaalam hata wa TEHAMA.
Mheshimiwa Spika, nchi za nje zinashindwa kufanya biashara na sisi kwa sababu hatuna utaalam huo. Mazingira ya rushwa, ufisadi na urasimu katika kufanya biashara, haya mambo hatu-deal nayo, matokeo yake tunaanza kuwalaumu Kenya, tunailalamikia Kenya, Kenya wanatuzidi, wametutangulia. Is that their problem or our problem?
Mheshimiwa Spika, pamoja na haya mambo yote ambayo Serikali ilileta wataalam hapa ambayo nakubaliana nayo kwamba lazima tuwe waangalifu, lakini lazima tuji-position mahali ambapo tuwe na uwezo wa ku-compete Kimataifa, siyo kulialia. We are like babies, every time tunalia, Kenya wametutangulia. Kwani wewe kutanguliwa unaona tatizo gani? Tulipata uhuru kwa pamoja; kila siku tunalialia Kenya wajanja, Kenya wajanja. Hapa Tanzania tunalalamika, Kenya wajanja; ukienda kwenye aviation, Kenya wanatuzidi; hata hapa Tanzania, wao wako zaidi.
Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye tourism, Kenya wametuzidi. Tunalialia. Hatuandai watu wetu, hamweki mipango madhubuti ya kuandaa watu wetu kwenye mazingira ya kibiashara, tunabaki kulialia, mwisho wa siku tunakuwa kwenye mkia.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Kaijage.
Si Kaijage jamani!
MBUNGE FULANI: Mwijage!
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwijage, nakushauri, hivi viwanda vyako vya kwenye mabegi na kwenye mifuko ni kweli hatutapeleka bidhaa Ulaya, haiwezekani. Ni lazima tutengeneze mazingira. Mnalalamikia Kenya eti viwanda vya Wazungu viko Kenya, kwa nini nyie msilete viwanda vya wazungu hapa? Kwani si Watanzania wataajiriwa? Hiyo Dangote ni ya Mtanzania? Si ni Mnaigeria amekuja hapa Watanzania wanaajiriwa? Tusitafute visingizio tunashindwa kujipanga wenyewe, tunashindwa kutengeneza mazingira mazuri, halafu inapokuja mikataba hii tunaanza kulaumiana.
Mheshimiwa Spika, kubwa zaidi, nimemwona Mheshimiwa Hawa Ghasia hapa, mazungumzo mengine anayozungumza siyo ya kidiplomasia; ya kusema watu wengine tuna- support kwa sababu ya ushoga, hii siyo lugha za kidiplomasia. Tanzania siyo kisiwa, tunahitajiana vizuri sana.
Mheshimiwa Spika, la pili ambalo tunatakiwa tujue, kwa nini Kenya wamesaini? Lazima tujue kwa nini Kenya wamesaini? Haya masuala ya kidiplomasia ni vizuri tukatoa michango ya kidiplomasia kwa sababu tunahitajiana na watu wengine. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, leo wakenya wamesaini, Watanzania tunakaa pembeni; lakini kumbuka kuna siku kutakuwa na jambo ambalo Watanzania tutakuwa na faida nayo kubwa, lakini kuna uwezekano tukamhitaji Kenya au Rwanda. Wao watakapochomoa, itakuwaje? Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo ni lazima tujadiliane kama Taifa, siyo tukiwa blind; lazima tujadiliane tu-dialogue.