Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Spika, juzi nilisema hapa kwamba biashara ni vita. Nasikitika sana kwamba nature ya mjadala ambao unaendelea Bungeni ni kama watu ambao tunaenda vitani, halafu tunanyoosheana silaha.
Mheshimiwa Spika, inapokuja kwenye masuala ambayo nchi inakwenda kupambana na wengine, jambo la kwanza ambalo ni lazima tulifanye, wote lazima tuwe kitu kimoja. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, siridhishwi kabisa na nature ya mjadala, kwa sababu hatuoni aibu kutofautiana katika jambo ambalo huko tunakokwenda tunakwenda kupigwa na wenzetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nitawaambia kitu kimoja, why Kenya has signed? Kwa wale ambao labda mtakuwa hamfahamu, why Kenya has signed an EPA kinyume na maagizo ambayo Wakuu wa nchi wa Afrika Mashariki wamekubaliana? Why has they signed? Maua! Biashara ya maua ndiyo imewafanya Kenya waseme to hell with EAC, sisi tunasaini. Maua tu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama una nchi kama Kenya yenye uchumi mkubwa zaidi ya Tanzania, inakuwa tayari kuhatarisha EAC kwa sababu ya maua, lazima tujiulize mara mbili mbili. Hii mnarushiana mishale hii, hili siyo jambo la chama kimoja hili. Siyo jambo la CCM, siyo jambo la CHADEMA, siyo jambo la CUF, siyo jambo la ACT-Wazalendo, hili ni jambo la Tanzania. Kwa hiyo, naomba tutakapoendelea na mjadala huu tuitazame nchi, tusijitazame sisi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuna mambo sita muhimu ambayo yanatufanya sisi kama Tanzania tusite kuingia kwenye mkataba huu. Jambo la kwanza wanaita ni asymmetrical liberalization. EU wanasema sisi tuna-liberalize bidhaa zenu zote; nanyi tunawaruhusu kidogo kidogo, mta-liberalise asilimia 90 ya bidhaa zote na asilimia 10 ya bidhaa za kilimo. Wazungu wanasema, devils is in the details. Hiyo asilimia 10 ya bidhaa za kilimo ni nini?
Mheshimiwa Spika, ukienda kuangalia kwenye mkataba unakuta kwamba sisi tunaweza tukauza kila kitu kule, tukawabana wao waingize asilimia 10 tu, lakini ndani ya zile bidhaa 10 kuna bidhaa za mazao ya mihogo. Mazao ya mihogo ni nini? Starch kwamba sisi leo tunaweza tukawauzia wao mihogo (raw), wao wakatuletea starch. Ndivyo mkataba ambavyo upo. Kuna mazao mengi sana, ndiyo maana nasema, devils in the details.
Mheshimiwa Spika, wanatuambia kwamba hakuna export taxes, nini maana ya hii? Maana yake ni kwamba leo mkitaka msiuze korosho ambayo ni ghafi, mnataka muuze korosho iliyobanguliwa, EU wanasema usiweke kodi kwenye korosho ghafi. Sisi sera yetu ya kibiashara ni kwamba ili kuhakikisha watu wanabangua korosho, tunaweka kodi kwenye korosho ghafi.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa mkataba huu, ili tufanye hivyo, lazima kwanza tuombe ruhusa kwa European Union. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lingine ni ngozi. Ni kwa nini nchi ya Ethiopia imekataa katakata hata ku-negotiate na European Union? Kwa sababu Ethiopia wamesema sisi tunataka kujenga kwanza uwezo wetu wa ndani, tukishaweza kushindana na ninyi, tutakuja ku-negotiate tuweze kuwa na mkataba, hiyo ni Article 14.2. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuna jambo hapa ambalo limekuwa likiongelewa, lakini haliwekewi details; revenue loses. Kwa sababu, unapozuia export taxes na unaporuhusu bidhaa za European Union kuingia nchini bila kodi, maana yake ni kwamba, hutakuwa tena na import taxes ya bidhaa zote zinazotoka European Union, huta-charge excise duty kutoka bidhaa zote zinazotoka European Union, hauta-charge VAT kwenye bidhaa zote zinazotoka European Union…
Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba niongezewe muda kidogo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kitakachotokea tutapoteza. Hata kwa East Africa nzima tutapoteza Euro bilioni 3.6, zaidi ya shilingi trilioni nane. Kwa Tanzania peke yake tutapoteza dola milioni 853. Hesabu hizi zimefanywa na European Union wenyewe. Sasa nini ambacho kilitakiwa kifanywe?
Mheshimiwa Spika, kulitakiwa kuwe na mfumo wa kuweza kufidia hiyo loss. EU wamekataa huo mfumo wa kufidia loss. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya muda, naomba nipendekeze baadhi ya vitu. Moja, itakuwa ni faida kubwa kwa nchi yetu, kama mkataba wa namna hii ukisainiwa na Afrika nzima yaani kuwe na Continental Free Trade Agreement ambayo ndiyo iingie mahusiano na European Union. Kwa hiyo, nilikuwa nataka katika moja ya mapendekezo yetu, ushauri wetu kwa Serikali ni kwamba Tanzania itumie nguvu yake ya kidiplomasia ku-rally nchi nyingine za Kiafrika ili mkataba huu uondoke kwenye individual regional groups ambazo tayari zimeshasambaratika, tuwe na continental approach dhidi ya European Union. Faida yake kubwa hii ni kwamba, itasababisha tuwe na free trade area within Africa na tuwe na mahusiano na nchi hizo tukiwa na ukubwa kiasi hicho. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lingine ni lazima tu-negotiate; yaani moja ya maagizo ambayo Bunge linatakiwa litoe kwa Serikali, ni ku-negotiate compensation mechanism ya revenue losses, kwa sababu ukiingia mkataba wa namna hii, kuna trade diversion. Zile bidhaa ambazo tungeweza kuziagiza kutoka nchi nyingine, zikipewa preferential treatment, bidhaa za EU maana yake ni kwamba zinapotea. Kwa hiyo, ni lazima tuwe na compensation framework. Bila hiyo compensation framework, sisi ndio ambao tutaingia kwenye shida zaidi.
Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie hii point ya mwisho tu.
Mheshimiwa Spika, Mawaziri wamshauri Rais. Kwa kuwa sasa hivi tupo kwenye hali ya juu sana ya majadiliano ya jambo hili, tunahitaji a political commissar ambaye akilala, akiamka anaangalia hii mikataba ya kibiashara ya Kimataifa tu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sasa hivi Wizara ya Viwanda na Biashara ina Waziri tu, haina Naibu Waziri. Waziri akihangaika na kututafutia viwanda, atapoteza focus ya kuhangaika kwenye negotiation.
Kwa hiyo, tuiombe Serikali, sisi hatuna mamlaka ya kumwagiza Rais, lakini tumshauri kwamba tunahitaji msaidizi wa Mheshimiwa Mwijage pale (political commissar) ambaye kazi yake yeye na apewe instrument maalum ya ku-deal na hili jambo ili kuhakikisha ya kwamba at all time tuna mtu ambaye yuko dedicated kwenye jambo hili tu, wakati Waziri anaangalia kwa ujumla wake masuala mengine ya viwanda na kadhalika, ili tuweze kuwa na nguvu ya kuweza kwenda kushindana na kujadiliana na wenzetu.
Mheshimiwa Spika, nakushukuru na ahsante sana.