Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Tunachojadili hapa tatizo letu ni mkataba au ni terms za mkataba? Tukigundua tofauti, kama tunaona terms za mkataba hazitu-favour, tunafanya nini tuwe na terms zinazotu-favour? Tatizo letu ni kukataa au tatizo letu ni ku-argue? Are we arguing or we are complaining? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tunachofanya tujitambue kama Taifa, are we in a position to set terms tunazozitaka? Hicho ndicho tunachopaswa kufanya kama Wabunge. Tusitake kukaa hapa kwa vile watu wamekuja, wakatuambia mkataba ni mbovu, basi kila anayesimama anasema mkataba ni mbovu. Let us talk of the issues, mkataba ni mbovu katika lipi? Mkataba ni mzuri katika lipi? Hapo tuta-set tofauti ya kuwa na Mbunge na kuwa shabiki wa kuambiwa sema moja, mbili, tatu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ya pili tunayopaswa kujua, huu mkataba unasainiwa between blocks; tunaweza kuongea na member states wetu katika block yetu ya East African countries tuka-negotiate the terms. Wanashindwa kukaa kuongea na sisi kwa sababu we always have fear of the unknown. Tuna-fear, tuna-complain, hatuko comfortable hatujielewi. Kenya ikiongea tunajua wanashirikiana na mabepari kwa ajili ya ku-colonize. Taifa lingine likiongea sisi hatuwezi kujisimamia kama nchi? Tutaanza lini kujisimamia? Tuwashawishi sasa member states, the East African blocks twende forward tuwaambie these terms so far are not favourable, we want (a), (b), (c). (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama haitoshi, swali ambalo tunapaswa kuongea leo, tuna bilateral relationship between Kenya, Uganda na nyingine East Afican States, tunakaa humu ndani, tunawa-brand Kenya kama watu wanaotaka watu-colonize halafu Mheshimiwa Rais anaenda kushinda Kenya, anasema those are our brothers and sisters. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, nakumbuka katika hii summit ya East Africa, Museveni aliwaambia, let us not punish the Kenyans simply because they are one inch taller. Tutakuwa tunafanya makosa. Tuongee na Kenya with terms, you guys look here, kwa kusaini huu mkataba, sisi tutapoteza kwa kiwango hiki, mnaonaje? Tunaweza ku-negotiate vipi tu-compensate hii deficit? Instead of arguing, tuna-complain humu ndani. Tujipime upya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kukataa kwa matusi na vijembe, vinahatarisha hata urafiki wetu na Kenya, Uganda, Rwanda na bado hatuna terms tunaleta mezani, tunataka moja, mbili, tatu. Niambieni tunataka nini zaidi ya ku-complain? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, tukimaliza sasa tujiulize swali, tunagombana na Kenya au tunagombana na Europen Union? Tukikaa sasa kama block ya East Africa ndiyo tutaenda kupambana sasa na European Union between the terms we want to have. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hiyo ndiyo tofauti tunayochangia hapa, tuseme tuna-complain kuhusu mkataba; tunasema tusaini mkataba au tusaini terms? Tusisaini terms; tusisaini mkataba, tusaini terms. Tuwaambie we want (a), (b), (c). Tukizileta hapa, tutasaini na siyo mkataba tunaousema.
Mheshimiwa Spika, nadhani watakuwa wameelewa. Tutofautishe ushabiki na issues. Let us talk of the issues, tusiongelee propaganda.
Mheshimiwa Spika, nakushukuru.