Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote niseme tu kwamba mimi na timu yangu ya wataalam pamoja na Naibu wangu, tumepokea maoni yote ya Waheshimiwa Wabunge waliyoyatoa kuhusu Wizara yetu ambayo wangependelea yaonekane kwenye Mpango na tutakaa na wenzetu wapokee Mpango wetu kama Wizara waweze kushirikisha kwenye Mpango mkuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba pia tutatumia mawazo ambayo tumeendelea kukusanya kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge na leo hii tunakutana na Wabunge karibu wa sekta zote, nadhani Bunge litahamia pale Msekwa. Lengo letu tunapotoka hapa, tunavyokwenda sasa kukamilisha jambo zima la Mpango tuwe na mawazo kwa upana yanayotokana na uwakilishi wa wananchi ambao ni Wabunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nirejee tu kusema kama mnataka mali mtaipata shambani na leo hii niende kwa kusema kwamba tunavyotawanyika hapa katika maeneo ambayo yanahusu sekta yangu, wale ambao wanatusaidia walioko mikoani na wenyewe watusaidie na nitazungukia katika maeneo hayo kuweza kuona utekelezaji wake.
Jambo la kwanza, tunajua utaratibu wa mgawanyo bora wa ardhi unaanzia ngazi ya kijiji, unakwenda mpaka ngazi za mikoa na baadaye unaenda ngazi ya Mheshimiwa Waziri kwenye Wizara yake ambako kuna timu ya mpango bora wa matumizi ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nielekeze ofisi zetu za Wakuu wa Mikoa wachukue hatua ya kuzungukia kila eneo, wapange maeneo ambayo wanayabainisha kwa ajili ya ardhi ya mifugo na kwa ajili ya ardhi ya kilimo na nitapita kuzungukia maeneo hayo ili tukishayatenga tuweze kuwa na maeneo ambayo yanajulikana matumizi yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti mpaka sasa nchi yetu ina hekta zaidi ya milioni 60 ambazo zinafaa kwa mifugo, lakini eneo ambalo linahusika kwamba hili limepimwa na linalindwa kwa ajili ya mifugo ni 2% tu. Kwa hiyo, tunahitaji maeneo haya yapimwe na yabainishwe matumizi yake na kama shida ni gharama tutaweka hata beacon za asili. Nakumbuka vijijini tulikuwa tunapanda hata minyaa, inajulikana kwamba huu ni mpaka. Tutaweka hivyo ili wakulima na wafugaji wasiendelee kuuana katika nchi ambayo ina wingi wa ardhi ambayo inaweza ikapangiwa matumizi na ikapata matumizi bora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niseme, mwenzangu wa Wizara ya Viwanda, kama tutakuwa tumeweka vizuri kwenye upande wa mifugo, pakajulikana wapi pana mifugo kiasi gani, itakuwa rahisi yeye kushawishi mtu aweke kiwanda cha maziwa, kiwanda cha nyama au kiwanda cha ngozi. Hili linawezekana kwa sababu katika mazingira ya kawaida, Wizara inawaza kutumia wafugaji wetu hawa hawa kuwa chanzo cha kwanza cha watu wa kufikiriwa kuwa wawekezaji kwenye mifugo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu ambaye ameweza kufuga kwa shida akapata mifugo 2,000, nina uhakika akitengewa eneo na likawa na miundombinu na huduma za ugani, ni mmoja anayeweza kuwa mwekezaji mkubwa, lakini wakati ule ule wafugaji wetu wakawa wamehama kutoka katika ufugaji wa kuzungukazunguka na kwenda kwenye ufugaji wa kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kilimo nilishasema kwamba, tumekusanya mawazo ambayo tutayatumia katika kuondoa zile ambazo ni kero, ambazo Mheshimiwa Rais alishawaahidi Watanzania kwamba atazifanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengine ambayo yamekuwa yakiwasumbua wananchi ni upande wa masoko. Tutaimarisha kuanzia upande wa ubora katika uzalishaji ili kuweza kujihakikishia ubora wa masoko na niwahakikishie kwamba, katika mazao mengi yanayopatikana hapa Tanzania soko lake bado kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mdogo, zamani tulikuwa tunajua mahindi ni zao la chakula au mchele ni zao la chakula, lakini niwaambie Waheshimiwa Wabunge, hivi tunavyoongea, zaidi ya watu bilioni 7.3 wanaoishi hapa duniani, nusu yao wanategemea mchele kama chakula na 40% wanategemea kula ngano kama chakula na zaidi ya bilioni moja wanategemea mahindi kama chakula. Kwa maana hiyo, hilo soko ku-saturate bado sana. Tuna mahali pa kuuzia mchele wetu, licha ya sisi wenyewe kwanza bado tunahitaji kwa ajili ya chakula.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu jambo moja kwenye mazao. Kumekuwepo na unyonyaji mkubwa ukifanywa kwa wananchi wangu, wa upande wa sheria atasema anayehusika na sheria hizo na usimamizi wake, wa upande wa Viwanda pamoja na upande wa TAMISEMI. Wanunuzi wanapokwenda kununua wananunua kwa hiviā€¦..
ili wananchi wauze kwa vipimo vinavyojulikana. Zimeshakwisha?
MWENYEKITI: Ndiyo, muda umekwisha.
WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Mpango na naunga mkono hoja iliyoko mezani kwetu. Ahsante sana.