Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa nafasi hii na mimi nichangie kwa ufupi kwenye pendekezo la mpango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa tumesikiliza michango ya Waheshimiwa Wabunge, na kimsingi mingi imekuwa ikitushauri namna ya kuboresha baadaye mpango wakati tunautayarisha, kwa hiyo kazi waliofanya ni kazi ya kwao kimsingi wanashauri serikali wao kama wawakilishi wa wananchi tumepokea mapendekezo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja kuhusu kilimo, mifugo na uvuvi nyingi zimejikita katika kuonesha kwamba mapendekezo ya mpango hayajajikita kwa undani kuhusu kilimo. Tunapokea mapendekezo ambayo yametolewa, lakini tufahamu kwamba hata baadaye tukiwa na mpango bado itabakiwa ni frame work haiwezi ikaingia kiundani kila eneo la kilimo, mifugo na uvuvi, baadaye itabidi tujenge mikakati mahususi kuhusiana na eneo moja moja la sekta hizo.
yamezungumzwa mengi kuhusu hali ya uchumi katika kipindi ambacho Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano tuliahidi kuleta mabadiliko, tena mabadiliko makubwa, hatutegemei mabadiliko makubwa yatokee lakini tusihisi au tusione mabadiko yenyewe. Kwa hiyo tofauti ambayo tunaiona sasa ndio ushahidi kwamba kuna mabadiliko. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani leo hii tukasema kwamba tunashughulikia kuhusu ubadhilifu na matumizi mabaya ya fedha za Umma lakini hapo hapo pale wanaposhughulikiwa wanaofanya hivyo tukalalamika kwamba ni kitu kibaya, haiwezekani. Lakini vilevile haiwezekani kwamba tunategemea Serikali ilete mabadiliko makubwa lakini sisi Waheshmiwa Wabunge hatutaki kuwa sehemu ya mabadiliko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahatma Gandhi alishawahi kusema be the change that you wish to see (kuwa sehemu ya mabadiliko ambayo unataka tuone). Naombeni Waheshimiwa Wabunge tuweni sehemu ya mabadiliko, tukubali kuondoka kwenye comfort zone zetu ili tuweze kuisaidia Serikali ya Awamu ya Tano kuleta mabadiliko ambayo tunaka, nashukuru sana.