Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa hii na kwa sababu muda ni wa dakika hizo ulizozitaja ambazo kwa hakika ni muda mfupi sana nichangie tu haya yafuatayo ambayo na amini yatatosha kwa muda huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza tunajadili mapendekezo ya Mpango wa mwaka 2017/2018. Mpango wenyewe bado haujaja lakini majadiliano haya ndiyo yanatarajiwa sasa yaboreshe mpango huo kabla hata haujaletwa hapa mbele yetu na ambao bado pia tutakuja kuuboresha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni Mpango wa Pili, wa mwaka moja moja kati ya ile mitano; na katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano tumejikita kwenye suala la kuelekea uchumi wa viwanda, na kila mmoja anakumbuka kwamba viwanda tunavyovizungumzia hapa zaidi ni vile ambavyo moja kwa moja vinahusiano na kilimo, kwa maana ya malighafi lakini pia kwa maana ya kuongeza thamani mazao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kuzungumzia kilimo ambayo maana yake ni kwamba huwezi kuzungumzia viwanda kwa mwelekeo tunaouzungumzia bila kuzungumzia hali ya hewa. Hapa nataka kuipongeza Serikali baada ya kuleta mapendekezo haya ambapo kwenye kitabu tulichonacho hapa ni ukurasa wa nane kwenye misingi ya mpango na bajeti kati ya misingi ile saba inayotajwa pale moja wapo ni hali ya hewa. Hapa naipongeza sana serikali kwa kuzingatia hali ya hewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya hewa kwa upana wake, maana yake ni pamoja na uoto wa asili ambayo ni misitu, lakini pia ni pamoja na suala zima la tabia nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka tu niwakumbeshe Waheshimiwa Wabunge, kwa sababu wengi walizungumza pale awali wakitaja changamoto mbalimbali kwenye sekta hii ya mali asili. Mimi nataka niwakumbushe tu kwamba kwa hali hii ilivyo sasa ni mbaya, na hiyo inatokana na ukweli kwamba tumeharibu sana uoto wa asili, kwa maana ya kwamba misitu imeharibika sana. Tumeshatoa takwimu tukisema jumla tuna hekta milioni 48.1 za uoto wa asili, lakini hizo zinapungua kidogo….
Mheshimiwa Mwenyekiti, sentensi ya mwisho ni kwamba tutakapokuwa tunajadili mpango pale utakapokuja kule mbele ya safari, kama ambavyo mapendekezo haya yalivyopendekeza, tuzingatie hali ya hewa, na kwahiyo tuzingatie sana suala la kuhakikisha tunazilinda mali ya asili na kuzingatia masharti ya maliasili.