Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa sababu ya muda kuwa mfupi nitachangia kama mambo mawili au matatu kwa ajili ya kuisaidia Serikali kwenye huu mpango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ninalokwenda moja kwa moja kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ni kwamba ukipitia hotuba yake, hususan maeneo ya kipaumbele kwa mwaka 2017/2018 utagundua hapa kuna maeneo mengi kweli kweli, hii miradi ya kielelezo ipo karibu kumi na kitu, ukienda kwenye kila sekta wameweka miradi mingi sana. Ninalisema hili kwa sababu unajua standard za priority unazifahamu, ukitaka kuweka vipaumbele maana yake unatakiwa uchague viwili, vitatu, maximum vitano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukishakuja na vipaumbele zaidi ya kumi na huu unakuwa ni uwongo, ni jambo ambalo halitekelezeki. Kwa hiyo, jambo ambalo nataka kuishauri Serikali, ili waondoe ugomvi na Wabunge, dunia hii ilivyo hata ufanye nini watu hatuwezi kuridhika lakini namna ambavyo unaandika unataka uridhishe, huku na huko tunapeleka mradi, kwa fedha gani? Kwa hiyo, at the end of the day, mwisho wa mwaka ni kwamba tutawalaumu tena mwakani kwa sababu haitekelezeki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi wewe mwenyewe unajua, miradi sisi tangu tunasoma shule ya msingi, mfano makaa ya mawe Mchuchuma na Liganga, yaani ipo tu kila mwaka hai-mature, every year hai-mature, unaweka miradi ya kielelezo, mwakani tutazungumza yale yale, miradi kama hii wewe unaondoa unapeleka kwenye Wizara husika itekeleze katika ile miradi ya miendelezo ya kila siku. Unaweka mradi unaandika kwa mfano, uanzishaji wa Kituo cha Kibiashara cha Kurasini, wawekezaji hawapo, wale Wachina walishaondoka, sasa ukishaweka kielelezo maana yake what are you doing?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo unakuta ni miradi ambayo tunajua kabisa ikifika mwakani tutamweka kwenye 18 Mheshimiwa Mpango atalalamika tena, jamani mimi mgeni kwenye Wizara mnanionea, mambo haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ushauri wangu kwenu Wizara nendeni mkachague miradi mitatu, minne, unajua hata ukitekeleza hapa kwa asilimia 100, 98, watu tutakupongeza, huo ndiyo utaratibu wa kuongoza nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hilo nililiona kwa sababu nikaona kabisa kwamba sasa tuache kuwapiga tuwape solution. Sasa changamoto ni kwamba mkiamua kuyapuuza up to you, lakini hiki ninachokwambia, leta mitatu, minne, nina uhakika mnaweza kutekeleza kwa kiwango cha pesa ambacho kinakusanywa, hilo linawezekana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, utekelezaji wa mpango umekuwa ukikutwa na changamoto nyingi sana, na changamoto kubwa ya utekelezaji wa mpango ni fedha. Asilimia kubwa ya mambo ambayo tumekuwa tukikutana nayo hizi fedha mara nyingi zinahusu wahisani, sasa wahisani ndio hao, leo wanaweza wakasema mwakani tutailetea Serikali dola milioni 900 na ikifika mwakani mmekwaruzana kwa sababu fulani wanasitisha ile misaada, na ukija Bungeni sisi kama Wabunge tunakwenda kuwaambia wananchi kwamba Serikali ilitenga kiasi hiki kwa ajili ya mradi huu, wahisani wamejiondoa, anayebeba lawama baada ya hapo ni Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hii miradi ya msingi ambayo tunataka kupeleka kwenye utekelezaji lazima kwanza Serikali iwe na uhakika imepata fedha kwanza, halafu ndiyo inaleta kwamba huu mradi tunakwenda kuutekeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninachoshauri ni kwamba mnaweza mkakopa huko, mkishakopa ndiyo unakuja hapa. Nazungumza kama Waziri wa Viwanda na Biashara, kiwanda hiki kitaanza kujengwa kufikia mwezi wa kumi, hela ipo kwenye akaunti, usizungumze kwamba jambo litafanyika wakati hela haipo huo tunaita ni uongo na ni jambo ambalo halitekelezeki. Huu ni ushauri ambao naipa Serikali leo, ikiyafuata haya mambo mwakani hamtalaumiwa, lakini msipoyafuata haya mambo mtaendelea kulaumiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, nataka nizungumzie TRA, kwenye ukusanyaji wa mapato TRA wamekuwa wakilalamikiwa sana. Leo ukisikia kila kona ya nchi TRA wanakamata, sibishani na watu wanaokwepa kodi, nataka TRA wakusanye kodi, lakini kinachofanyika kule nje, wanaenda kwa mtu, ana biashara yake wakimkuta mtu kwa mfano hajalipa kodi wanamkamata, wanafunga biashara yake, sasa matokeo yake nini? Unapomfungia mtu biashara yake na unamdai kodi, maana yake yeye mwenyewe hapati kipato, Serikali inakosa fedha kwa kumfungia yule mtu biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wale watu wamekopa mabenki wanashindwa kurudisha mikopo, kwa hiyo, hapo TRA kumfungia mfanya biashara ni kukomoa Watanzania, ni mambo ya kawaida ni madogo madogo sana yanaweza kutekelezeka humu ndani. Serikali inachotakiwa kifanye wale wote wanaodaiwa kodi watengeneze utaratibu waweke kama malipo benki, benki ukishindwa kulipa fedha zako zikiwa nyingi wanakuambia tunakupunguzia ama tunakuongezea muda wa kulipa, utakuwa unalipa kiasi hiki in installment. Sasa TRA wanataka wao ….
MHE. DAVID E.SILINDE: Haya ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, leo nilikuwa nashauri kwa sababu mmepigwa sana na ukiona watu wanasema sana ujue kuna tatizo sio kwamba watu wanawaonea.
Kwa hiyo, ushauri wangu naomba hayo mambo matatu myafanyie kazi mwakani hatutawalaumu, mkiendelea kutaka kufanya yote kuridhisha kila mtu hamtafanikiwa. Ahsante sana.