Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi ya kuchangia Mapendekezo ya Mpango uliopo mbele yetu. Kwanza nichukue fursa hii kuipongeza sana Serikali kwa kutendo cha kudhibiti matumizi hasa kwenye taasisi zake na mashirika ya umma. Kubwa kuliko lote hasa kitendo cha kuhamisha akaunti zote za taasisi hizi kuwa BOT, ni kitendo ambacho ni cha kizalendo sana na hili nalisema kwa kinaga ubaga na mifano ipo hai. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kuna baadhi ya wenzetu wanasema kwamba hali halisi ya maisha yamekuwa magumu kwa sababu ya kitendo hiki, siyo kweli. Siyo kweli kwa sababu hizi benki zilianzishwa, kazi yake ni kuhudumia wateja, kutoa mikopo kwa wafanyabiashara. Lakini hujuma zilizokuwa zinafanyika nitoe mfano mmoja tu wa taasisi moja kama ya bandari, yenyewe iliweka bilioni 440, kwenye fixed account kwenye mabenki mbali mbali kwa rate ya 3.5%, bilioni 440. Halafu yenyewe tena ikaenda kukopa kwenye benki hizo hizo bilioni 100 kwa ajili ya miradi yake ya maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mtu hapa, baada ya Serikali kuona hujuma hizo, kupeleka hizo akaunti BOT anasema Serikali imenyonga wafanyabiashara, siyo kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna taasisi nyingine hizo hizo, hii mifuko yetu ya kijamii, inakusanya shilingi bilioni 38 kwa mwaka, shilingi bilioni 27 matumizi kwa sababu fedha zipo tu za kutumia, inachangia kwenye mfuko shilingi bilioni mbili tu kwa mwaka mzima, leo Serikali imeona hujuma hizo imepeleka hizi fedha zote zikapate udhibiti BOT mtu anasema wafanyabiashara wamenyongwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali kwa kitendo hiki cha kudhibiti matumizi yasiyokuwa ya lazima na ovyo ambacho sasa tuiombe tu Serikali ifanye mfumo mzuri ambao kama hizi benki zipo ziende sasa zikakope kule BOT kwa rate inayokubalika ya sokoni siyo ile ya kiwizi wizi ya 3.5 halafu fedha nyingine zinaenda kwa wajanja wachache. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa sababu huu unasema ni wizi alafu hizo hizo benki zilikuwa zinaikopesha Serikali kwenye treasure bill, Serikali ikiwa na tatizo inakwenda kukopa kwenye benki zile zile kwa rate kubwa zaidi ya asilimia 15, 20. Kwa hiyo, niwaombe Serikali hapo msilegeze, msimamo ni huo huo ili kwamba tuwe na nidhamu katika matumizi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu wa pili kuhusu makusanyo hasa kwenye TRA, nilikuwa naomba Waziri Mpango katika mapendekezo ya kuongeza tax base, kweli tumepata muhamasisho wa Rais na watu mbalimbali kwamba watu wajitolee kwenda kulipa kodi kwa hiyari, lakini kitendo cha Mtanzania, wengi wanahofia ukisema leo nataka kuanza kulipa kodi, TRA sasa hawaanzi pale, watakupa hizo kodi miaka kumi ijayo hata kulipika hazilipiki. Ni sawa sawa sasa wanakwenda kufilisi, matokeo yake watu wanaogopa na watu walipakodi wanaendelea kubaki walewale, ni kitu ambacho hakitaisaidia Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri tu, kama kuna uwezekano toweni muda maalum kwamba watu wajitokeze kulipa kodi ili muongeze wigo wa tax base, lakini mkasamehe hayo makando kando ya nyuma ili watu waanze kulipa kuanzia hapo kwenda mbele. Tutaongeza wigo mpana wa kulipa kodi kuliko kung’ang’ania kusema mpitie makando kando hayo watu hawana risiti, hawana uthibitisho zaidi ya kuwafilisi, matokeo yao watafilisika, hamtakusanya tena hizo kodi uko mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mwingine sasa hivi kwenye makusanyo hayo ya kodi…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, naunga mkono hoja.