Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia huu Mpango wa Maendeleo. Nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa sababu ukiuangalia kwa ujumla mpango huu, nimeusoma vizuri na pia niseme kwamba nimechangia kwa maandishi kwa sababu ya muda. Mpango huu ni mzuri kwa sababu mpango huu ni muendelezo wa ule mpango wa miaka mitano. Kwa hiyo ukiusoma vizuri utaona kabisa kwamba uko mwendelezo mzuri, sasa kuna mambo kadhaa ya kufanya, ambayo nilikuwa napenda kushauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango huu umezingatia Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lakini pia umezingatia mpango wa maendeleo endelevu. Kwa hiyo, nilikuwa nataka ni- appreciate kwa kuona kwamba kwa kweli ukiangalia hali ya uchumi kwa ujumla kwa taarifa ilitolewa na BOT mwezi Agasti, utaona kabisa kwa performance ya bajeti ya Julai, maendeleo ni mazuri, kwa hiyo, ninampongeza sana Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende tu moja kwa moja kwenye ushauri, nilikuwa napenda nishauri mambo kadhaa, ambayo tumeyaona kama changamono na Waheshimiwa wengi wamechangia hapa. Ipo changamoto ya ukusanyaji kodi kwamba yako maeneo kama mpango unavyosema kwamba unakwenda kutazama sekta binafsi, lakini pia tumezungumza juu ya kuendeleza viwanda, lakini uko uhusiano mkubwa kati ya sekta binafsi na ukuaji wa viwanda na suala la ukuaji wa uchumi kwa ujumla. Kwa hiyo kuna mambo ya kuyaangalia hapa ili sasa tuweze kusaidia sekta, Mheshimiwa Waziri ajaribu kuangalia maeneo haya ya kodi, kwa sababu ukweli lazima wafanyabiasha na sekta binafsi walipe kodi. Lakini kuna maeneo ambayo ni ya kuyatazama ili kuweza kufanya ile tax compliance iwe ya hali ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija kuangalia kwa mfano, upenda wa VAT kwenye viwanda vyetu ambavyo vipo kwa mfano, viwanda ambavyo vinasindika mafuta, mashudu yale yamewekea VAT, utakuja kuona kwamba VAT register ni kama agent wa TRA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapokuwa na hii VAT kwenye uzalishaji wa kwanza utaona inavutia kuongeza bei na kwamba ule ushindani sasa wa bei unakuwa ni mgumu kwa product inayofanana na wenzetu nje ya nchi na hata kwa watumiaji wa bidhaa hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tulitazame hili suala la namna ambayo kodi itahamasisha ili ule ulipaji wa kodi, compliance iwe kubwa kwamba mtu alipe bila kushurutishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo lipo nilitaka nishauri, kumekuwa na tatizo hili la mzunguko wa fedha. Sasa nilikuwa najaribu kufikiria kwamba tulikuja na sheria ya bajeti ili mwezi ule wa saba kuwe na kiasi cha kutosha cha fedha kuweza kuendesha bajeti zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kunahitajika kutazama hili suala la cash flow management, Wizara ilitazame ili tunapokuja kupitisha bajeti mwanzoni mwa mwezi wa saba kuwe na flow nzuri ya fedha kulingana na uhitaji katika maeneo mbalimbali, katika Halmashauri zetu. Kwa hiyo, sikuona tatizo sana kwa sababu kama bajeti ipo na fedha inayotolewa iko within the budget, hapa hakuna shida, ila lipo suala la kuangalia ile flow ya pesa inayokwenda kwa ajili ya matumizi, kwa hiyo, Wizara hapa iangalie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mzunguko wa fedha, hili linaonyesha kwenye sekta ya fedha, Wizara ilitazame kwa sababu kunapokuwa na mabadiliko ya hizi sheria za kodi zilivyokuja, lakini pia mabadiliko katika taasisi zetu za kifedha, watu wanapata hofu ya kupeleka fedha katika hizi taasisi za fedha. Kwa hiyo, utaona kabisa kwamba zile deposit kwenda kwenye mabenki zimepungua kiasi kwamba ule mzunguko umepungua. Kwa hiyo, sasa BOT iangalie namna yaku-regulate ule mzunguko wa fedha ili tuione inaleta impact kwenye mzunguko na ukuaji wa uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uko uhusiano mzuri sana kati ya sekta binafsi na ukuaji wa viwanda, sasa uko umuhimu pia wa kuliangalia suala la kilimo. Kilimo chetu hakijapewa msukumo wa nguvu ili kuhakikisha kwamba sasa tunapata raw material za kutosha kuendesha viwanda vyetu. Ukija kuangalia kwenye zao la pamba, uzalishaji wa pamba umeshuka, katika msimu huu ununuzi wa pamba umefanyika kwa wiki mbili tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, utakuta sekta binafsi watu wana viwanda vyao vya kuchambua pamba vimesimama mtu ambaye alitakiwa kununua tani 60,000 katika msimu huu amenunua tani 14,000 utaona kabisa kwamba tuna dead asset, ziko asset za wafanyabiashara hazisaidii mchango katika uzalishaji. Kwa hiyo, Wizara itazame namna gani ya kuweza kusaidia haya maeneo ili tuwe na uwiano mzuri kati ya uzalishaji katika kilimo, uzalishaji katika viwanda vyetu ili tuweze kuhakikisha kwamba nchi yetu inapata fedha za kutosha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine Serikali ijaribu kuangalia kusaidia tuje tupate kiwanda ambacho kita-support hivi viwanda vidogo ambavyo vipo vinachambua pamba, tupate kiwanda kikubwa kwa ajli ya kutengeneza nguo ili pia sasa tuweze kuzalisha nguo za kutosha ili wananchi wa Tanzania waweze kupata nguo kwa bei ambayo inakuwa ni nafuu na kufanya kwamba hali ya uchumi iweze kuwa nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilitaka pia nimalizie kutoa ushauri kwamba tulipokuwa tumeanzisha mfumo wa usimamizi wa fedha tumekuja na hii concept ya accrual basis, sasa…
MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono, ninashukuru sana.