Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi ambayo nimepewa kuweza kuchangia hotuba hii ya Waziri wa Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niunge mkono hotuba ya Kambi ya Upinzani ambayo ilitolewa kabla. Katika mpango wa Serikali ya Awamu ya Tano ni Tanzania ya viwanda, nimepitia katika Mpango huo ambao umewasilishwa na nasikitika kusema kwamba, katika Mpango wote ambao umewasilishwa pamoja na umuhimu wa kukuza viwanda, sijaona ni kwa namna gani rasilimali watu imepangwa kusudi kusaidia kuendesha viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu mwaka jana katika ule Mpango kulikuwa na suala la kupeleka wanafunzi 159 wa petroleum and gas kwenda kusoma, lakini sioni katika mpango wa mwaka huu ni kwa jinsi gani tumefikia wapi na wale 159 kwamba wanatosha au tunahitaji ku-train watumishi wengine kwa ajili ya petroleum and gas.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mwaka jana Serikali iliahidi kwamba itajenga vyuo vinne vya ufundi katika mikoa mbalimbali lakini katika mpango wa mwaka huu Serikali haijaainisha kama bado tunaendelea na hivyo vyuo vinne vya ufundi, imekuja na mawazo mapya ya kutengeneza karakana, sijui miundombinu. Je, vile vyuo vinne ambavyo Serikali iliahidi itavijenga, imefikia wapi? Ingependeza zaidi kama tungeweza tukapata status ya yale ambayo yalisemwa mwaka jana tuweze kufuatilia kama kweli yanatekelezwa au la! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mikopo ya elimu ya juu. Kama nilivyosema juzi, hii taasisi ya mikopo ilianzishwa ili kupanua udahili si kupanua udahili tu na kusaidia wanafunzi ambao ni wahitaji, lakini tumeona mwaka jana, kwa bajeti ya juzi hakuna pesa iliyotolewa ya kutosha na kwa mpango huu ambao umewasilishwa inasemekana kwamba udahili utaongezwa na tuta-train watu wengi, kama ikiwa mpaka sasa hivi bajeti inayotoka hata haikidhi wale wanafunzi waliokuwepo, je, ni kweli Serikali itakuwa na hiyo pesa ya kuingiza kwenye mzunguko mwaka kesho?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ningependa Waziri anisaidie kujibu, kuna hii hoja ambayo imeshajitokeza kwamba kuna wanafunzi ambao wanaendelea wananyimwa mikopo, mimi nauliza busara ya kawaida tu inasema kwamba hawa wameshaingia kwenye mkataba na Loans Board na wamesaini mikataba ya jinsi ya kurudisha hiyo hela na leo Serikali inasitisha kuwapa mikopo hawa wanafunzi wanaoendelea, ni kwamba Serikali imekiuka utaratibu wake wenyewe wa kuwapa wanafunzi hawa mikopo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, busara ya kawaida ingekuwa kuendelea kuwapa hawa wanaoendelea, halafu mipango mipya au uhuishaji au utaratibu mpya ungeanza na hawa ambao ni wapya, ndiyo utaratibu tunaofuata. Ningependa kupata ufafanuzi kuhusu hawa wanafunzi wanaoendelea ambao walikuwa wanapewa mikopo na sasa inasitishwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu, ni suala la Watumishi wa Umma. Naomba ku-declare kwanza interest kwamba nilikuwa Katibu Mkuu Utumishi. Nasikitishwa kwa jinsi ambavyo watumishi wamekuwa wanatumbuliwa left and right. Utakuta Mawaziri wanatumbua japokuwa tangu majuzi kidogo wametulia, Ma-RC wanatumbua, DC anatumua, DED anatumbua, wakati tunajua kabisa Mamlaka ya nidhamu ni watu gani ambao Rais amewakasimu. Hii inapelekea watumishi kukosa imani, kukosa amani na kukosa ubunifu na matokeo yake Utumishi wa Umma ambao ndiyo injini ya maendeleo utashindwa kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Makada wengi ambao hawakuwepo katika Utumishi wa Umma kabisa wamewekwa kwenye maeneo ya utendaji ambayo inakwenda ku-compromise uadilifu na uimara wa Utumishi wa Umma. Utumishi wa Umma duniani kote unaishi zaidi ya Wanasiasa. Wanasiasa malengo yao ni miaka mitano tu. Utumishi wa umma ambao ni legelege hautaweza kutekeleza huu Mpango ambao unaletwa. Kwa hiyo, hili jambo ni lazima liangaliwe kwa ukaribu sana ili kusudi Watumishi wa Umma wapate imani na waweze kufanya kazi zao vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Local Government Reforms, Serikali Kuu imekasimu madaraka kwa Local Government na kati ya maeneo ambayo ilikuwa imekasimu ni property tax au kodi ya majengo, tumeona Awamu hii ya Tano imeanza tena kurudisha collection ya property tax kwa TRA. TRA walishashindwa siku nyingi na ndiyo maana ilihamishiwa Local Government.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kigezo gani ambacho Serikali imetumia kuhamisha tena property tax kutoka Serikali za Mitaa kuja TRA wakati walikwishashindwa na tunajua kwamba Serikali Kuu imekasimu madaraka kwa Local Government. Inawezekanaje umpe mtu madaraka, umpe na rasilimali watu, lakini ukamnyima rasilimali fedha ya kuifanyia kazi, wakati Local Government ndiyo ina mashule, Local Government ndiyo ina hospitali, Local Government ndiyo ina barabara, watafanyaje hizi kazi ikiwa resources Serikali Kuu imewanyang’anya? Hili ni janga la Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi mikubwa ambayo imezungumziwa. Makaa ya mawe - Liganga, Mchuchuma, reli ya kati, general tyre, hizi story za siku nyingi tangu nikiwa Katibu Mkuu, nimestaafu miaka mitano sasa bado hadithi ni ile ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Bado hadithi ni ile ile. Tunataka Mheshimiwa Mpango aje atueleze ni namna gani hili jambo litatekelezwa. Ahsante.