Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DAVID C. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kukushukuru kunipa nafasi ili niweze kuchangia Mpango wa Maendeleo. Yameshasemwa mengi sana na Wajumbe ambao wametangulia kwa hiyo nisingependa kurudia ningeenda kwenye some specific issues.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ambalo ninapenda kuliweka wazi na kulisemea ni suala la watu kulipa kodi. Kodi katika Taifa lolote ni kama vile nerves za fahamu za mwanadamu. Kwa hiyo, kodi kwa kweli lazima kodi ilipwe, hilo halina mjadala, hata mataifa makubwa ambayo wakati mwingine yanatusaidia kama wahisani au kwa mikopo zile ni kodi za wale wananchi, kwa hiyo, linapokuja suala la kodi kwa kweli kusiwe na mjadala kodi lazima zilipwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tuje namna gani sasa ya huo ulipaji wa kodi, nitaanza kwa kusema katika hali ya kawaida kabisa ukusanyaji wa kodi lazima uendane sambamba na elimu kwa walipa kodi. Leo hii wananchi wetu kwa kukosa ufahamu pale Mafinga mwananchi amedunduliza, ameuza gobo (mahindi yale ya kuchoma ambayo yanavunwa bado mabichi), amepata kibali amevuna mbao ameuza, amenunua gari lake labda kwa mtu “A”, keshokutwa TRA wanamkamata kwamba wewe bwana ulinunua hili gari hukulipa kodi, hukulipa capital gain, sawa ni sheria lakini mtu huyu kumbe hana ufahamu wa lile jambo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yeye akinunua gari, akaandikishana mkataba na aliyemuuzia akampa kadi yeye anaona ameshamaliza, sasa kumbe hata hawa walipa kodi wadogo wadogo hebu TRA sambamba na ukusanyaji twende na elimu pia ya ulipa kodi kwa sababu hata sisi wenyewe Wabunge wengi tunapotaka kama unafanya biashara masuala ya kodi lazima utatafuta mshauri wa kukuelekeza katika suala zima la kodi.
Kwa hiyo, tupeleke elimu kwa watu hawa sasa mtu huyu kama nilivyosema amenunua gari lake, ameamua kufanyabiashara ya kusafirisha watu, kumbe hajui ukitaka iwe gari ya biashara kuna taratibu zake pia za kikodi gari inakamatwa, ameshajimaliza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, TRA the way wanakuja yaani hawaji kwa ile elimu kwamba you are supposed to do this ili uwe katika njia hii hapa. Yaani wanakuja kwa namna ambayo ni ya ambush. Kwa hiyo, kama nilivyosema sipingani, kodi lazima ilipwe, lakini pia jitihada za kukusanya kodi ziende sambamba na elimu ya kuwaelimisha wananchi kulipa kodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hili hizi machine za EFD kwanza hazijasambazwa vya kutosha, lakini leo nilikuwa nasoma kwenye gazeti, Sheria ambayo sisi wenyewe of course tulipitisha kama hujadai risiti kuna fine utapigwa pale lakini mashine nyingi ninyi wote mashahidi unaenda, oh, mtandao uko chini mashine haifanyi kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Waziri hebu tusaidie hii ilikuwa ni deal ya watu au kweli wenye biashara mashine ni mbovu? Lakini shaka yangu kwamba hizi mashine yawezekana toka mwanzo hazikuwa mashine madhubuti. Sasa hawa wanao-supply tumejiridhisha kweli wana-supply mashine za EFD zinazotakiwa? Kwa hiyo, tunaweza tukajikuta siku tunashurutisha watu kumbe mashine yenyewe hatujazisimamia ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie, elimu ya kulipa kodi ina umuhimu wananchi toka lile tangazo la Mheshimiwa Magufuli na tangazo la kale katoto nipe na risiti, imewaingia watu mpaka watoto wangu nikinunua gazeti tu wananiambia baba mbona hujadai risiti? Lakini sasa kama elimu imeanza kuwaingia hivyo ya kudai risiti na mashine hazifanyi kazi kwa wakati, mtandao uko chini, je, tutafikia malengo ya Mpango? Kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri ulitazame hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni suala la Liganga na Mchuchuma, amesema hapa ndugu yangu asubuhi, Mheshimiwa Sixtus Mapunda. Mimi hujizuia sana kuleta mambo ya Ukanda, lakini katika hili naungana naye au kwa sababu liko Kusini?
Mimi natoka Nyanda za Juu Kusini, bahati mbaya inaweza kuwa bahati mbaya au nzuri nilifanya mazungumzo na Balozi wa China kwa ajili ya mambo ya jimbo langu. Kati ya kitu ambacho hata Ubalozi wa China unasikitika mojawapo ni suala kulegalega suala la Mchuchuma, kulegalega suala la Bagamoyo na Mheshimiwa Waziri katika kitabu chako umesema hii ni miradi ya vielelezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa yawezekana kuna watu wengine wamesoma zaidi, wanaufahamu wa mambo haya lakini pia ni vizuri sana kutumia elimu yetu kuhakikisha kwamba tunalisaidia Taifa kusonga mbele pale ambapo tumekwama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano naambiwa katika suala hili, yule mbia ambaye ana ubia pamoja na NDC fedha za kulipa fidia wananchi wa Ludewa kule kwa ndugu yangu zimeshapatikana na zipo. Lakini mgogoro unaambiwa upo kwenye power purchasing agreement, sisi tunataka tununue kwa senti saba za dola wao kwa senti 13; lakini ukiangalia mradi ule katika ujumla wake, lengo lake zile megawatt 600 ni katika kutusaidia sisi tupate umeme. Lakini mradi wenyewe katika ujumla wake kama alivyosema Mheshimiwa Mama Nagu unaenda kusaidia ku-stimulate viwanda vingine. Tunataka sisi kujenga reli hapa, hayo mavyuma tutayatoa kule. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri, nikuombe kwenye suala la Mchuchuma tulipokwama tuone tunatoka wapi tuweze kufanikisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine kwa kushirikiana na Wizara ya Mamboya Nje, tusiwe nchi ya kusaini tu ma-MoU, alikuja hapa Rais wa China mara baada ya kuapishwa ni nchi ya kwanza duniani kuitembelea tumesaini mikataba 16, juzi tumesaini na Morocco, je, follow up iko wapi ya kila mkataba tuliosaini utakuwa na tija kiasi gani, tumekwama wapi, nani amekwamisha? Ili kusudi dhamiraya mpango huu iweze kutimia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie muda wangu naona unaniishia kuhusu suala la kilimo, katika Mpango huu hakuna mahali popote palipo reflect suala la kilimo kama ambavyo Mpango wenyewe wa Miaka Mitano unasema. Sasa niombe tujaribu kuwekeza katika kilimo hiki na tusaidie pia Shirika la Maendeleo ya Viwanda vidogovidogo SIDO kwa ajili ya kitu kinaitwa knock down technology. Juzi tumeona wakulima wa nyanya wanauza nyanya ndoo mpaka shilingi 800. Sasa wakati tuna-deal na mamiradi makubwa hebu pia tuone namna gani tunaweza kukinyanyua kilimo kwa namna ya kawaida, tukashirikiana na SIDO, tukajenga viwanda vya kawaida, tuka-add value katika mazao ya wakulima ili kusudi hawa wakulima kweli waonekane ni uti wa mgongo wa Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho kabisa ni single custom territory watu wengi wamesema; na mimi kwa ufahamu wangu ningeshauri sana Congo DRC tuwape special treatment ndugu zangu. Sisi single custom territory tu-deal nayo na sisi hapa EAC. Lakini hawa watu ambao volume yao kibiashara ni kubwa hebu wao tuwape special treatment.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno haya nimalizie kwa kusema wako watu wanaosema pengine Mawaziri wanaogopa kumshauri Rais, sidhani kama kuna kitu cha namna hiyo. Hawa ni watu wenye confidence, wenye kujiamini katika kazi, tuwape nafasi…
MWENYEKITI: Ahsante.