Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianzie hapo alipoishia Mheshimiwa Lema, Bunge kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linao uwezo wa kumu- impeach Rais. Sasa kama tuna uwezo wa kumu-impeach Rais halafu watu tukimtaja Rais hapa mnatetemeka maana yake tunataka tukiuke Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Bunge pekee, ni chombo hiki pekee, waliotunga Katiba walijua kuna wakati Rais anaweza akakosea na hiyo mamlaka iko mikononi mwetu. Mimi nashangaa Wabunge tukimtaja Rais kama anakosea tutamui-impeach vipi kama anakosea anapoingoza nchi yetu? Kwa hiyo, hebu turudi kwenye senses zetu kwamba mamlaka hiyo tunayo na wala hatumuonei kama anafanya makosa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe sana Mheshimiwa Mpango, wengi wamezungumza mimi narudia na juzi nilisema na tunasema ukweli kwa sababu tunalipenda hili Taifa. Nikuombe sana unapoleta mambo yako hapa usilete kama vile upo kwenye lecture room kwamba unataka kutupa lecture. Sisi ni wawakilishi wa wananchi, wametutuma wananchi na ndiyo maana mnapoleta huu mpango hapa ni ili sisi Wabunge wote tuujadili vinginevyo msingekuwa mnaleta mngekaa nao huko Serikalini muendelee. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana ulipoleta, tena mimi tulikutana pale nje, mimi huwa nasema openly, tulikutana pale nje nikakuambia hizo kodi unazoleta kwenye VAT utaleta chaos, nikakuambia hizo kodi unazoleta bandarini utaleta taabu. Bandarini sikuwa na utaalam sana walau kwenye maliasili nilikuwa najuajua kidogo, lakini zimesababisha shida kubwa kwenye nchi yetu halafu hapa tunalindanalindana, tunafichamafichama kuelezana ukweli na mnamdanganya mfalme kwamba mambo yapo vizuri. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitabu chake hiki najua kanuni zinaeleza kwamba hatuwezi ku-review bajeti iliyopita kwa sababu haijapita miezi sita, lakini haya mambo yote uliyoandika yame-based kwenye bajeti ile iliyopita ambayo hata wewe mwenyewe Waziri hukuwepo hapa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu mpango unaouleta hapa haupo realistic kwa sababu Ilani ya Chama cha Mapinduzi aliyomaliza Mheshimiwa Jakaya Kikwete kipaumbele hakikuwa viwanda, hii sasa ya Mheshimiwa Magufuli inazungumzia viwanda. Huu Mpango wako umetuletea mambo ya DARTS na kadhalika ambayo ni mafanikio yaliyopita ya Mheshimiwa Jakaya Kikwete. Kwa hiyo, mpango huu haupo realistic, upo baseless, tunajadili kitu ambacho hakina miguu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Serikali hii kwa sasa tunapozungumza mipango Mheshimiwa Waziri Mpango lazima tuwe na watumishi ambao wana confidence. Amezungumza Mheshimiwa Lema hapa ukienda kwa watumishi wote wa umma hawana ujasiri katika nchi hii, mmewa-terrorize wote, hawana confidence, hawajiamini kila mtu akiamka asubuhi hajui kitu gani kitatokea. Haya mambo tunayopanga tutawezaje kuyatekeleza kwa watu ambao hawajiamini! Umma umeaminishwa kwamba watumishi wote wa umma ni wezi, wafanyakazi wote hawana ujasiri wa kukaa kazini, ile morale haipo kwa sababu kila mtu ni mwizi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, amezungumza vizuri sana Mheshimiwa Lema tukisema dhamira ya Mheshimiwa Rais ya kutaka kuleta mabadiliko na nidhamu katika nchi hii au ku-restore glory haipo tutakuwa tunasema uongo. Kuna mambo ambayo ameonyesha dhamira nzuri, wote tunakataa rushwa, wote tunakataa mambo mabaya ndani ya nchi lakini njia anazozitumia za kutisha watu na kuvunja sheria hizo ndiyo tunazozikataa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Ripoti ya Utafiti wa Amani Duniani iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Institute of Economics and Peace ya mwaka 2015, Tanzania ni moja ya nchi 64 duniani zinazokaribia hatari ya kuvunjika kwa amani kwa sababu ya ukandamizaji wa kidemokrasia. Sasa tusipokuwa na amani na kuheshimu na mipaka na mipango tuliyojiwekea wenyewe tutawezaje kusonga mbele na mipango hii mizuri? Hii nchi ni yetu sote, pale Rais anapofanya vizuri tutakubaliana naye, lakini mazuri yake yote anayoyafanya yanaharibika pale alipozungukwa na watu ambao hawamwambii ukweli. Sisi hapa tutamwambia ukweli, mtukate vichwa tutamwambia tu, kama yupo uchi tutamwambia upo uchi, we are not scared of him. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zitto amezungumza hapa Serikali hii haipo coordinated. Ukienda kwa mfano kwenye mipango yako hii hakuna mahali popote ambapo umezungumzia espionage (uchumi wa kijasusi). Wizara ya Mambo ya Nje ndiyo jicho la nchi ambapo mimi nashangaa katika mipango yako ya mwaka jana haikukuambia jinsi ambavyo Congo ni ya muhimu sana katika bandari yetu ya Dar es Salaam, Wizara ya Mambo ya Nje ilikuwa wapi? (Kicheko)
Leo Wizara ya Mambo ya Nje kama ni jicho, kama ipo coordinated ingeweza kusema unapopeleka mpango huu kwamba bandarini tutaongeza kodi kiasi hiki Mheshimiwa Mpango unakosea tutapoteza potential customers. Kama Serikali hii ipo coordinated ulipopandisha VAT kwenye mambo ya tourism Waziri wa Maliasili angekuambia you are wrong tunaenda kupoteza watalii. Hata hivyo, kwa sababu mkiamka kila mtu afanya la kwake, anawaza la kwake na mnashindana kwenda kujipendekeza kwa Magufuli matokeo yake ndiyo mnatuletea mipango ya ovyo ovyo. Tupo hapa kama Bunge, hampo coordinated ndiyo maana Mheshimiwa Kigwangalla anaweza akasema dawa zipo kidogo, Mheshimiwa Ummy anasema zipo za kutosha na Makamu wa Rais anasema hazipo, tumsikilize nani sasa, the same government! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri najua ni msomi, Mpango huu kuna tafiti nyingi ambazo hata rafiki yangu asubuhi amezizungumza hapa. Ukiangalia tafiti zilizofanywa na Taasisi ya Kimataifa ya GCI kuhusiana na mazingira bora ya uwekezaji Tanzania inashika nafasi ya 120 kati ya nchi 140 zilizotajwa kwenye uwekezaji huo. Ukiangalia moja ya matatizo tuliyonayo Tanzania nchi yetu imekuwa ni ya nne, mazingira ya uwekezaji hayajawa mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Tanzania inahesabiwa kwamba hatujawa wazuri katika matumizi ya teknolojia. Huu mpango hautafsiri ni namna gani tunapambana na hayo maeneo ili tutengeneze mazingira mazuri ya uwekezaji. Kwa hiyo, hizi tafiti zinaletwa halafu Mheshimiwa Mpango na wewe unaenda njia yako. Serikali nzuri na jasiri inaweza ikasimama na mimi ningekuwa wewe ningekuja hapa kwa sababu kimsingi hili joto tunaloliona mwezi wa sita mwakani litakuwa kubwa sana na inawezekana Bunge likaondoka na kichwa chako hapa. Inawezekana Mheshimiwa Waziri huu mpango labda ali-copy New Zealand au Australia, ni busara tu kuja hapa na kusema jamani this things it is not going to work here nili-copy mahali nika-paste hapa hai-work, tutaambizana ukweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo ambayo ni kweli tumeshindwa kuyafanya kwa visingizio mnavyovileta, lakini kuna mambo we told you, ulishupaza shingo ukakataa. Kuna data nyingi zinaonyesha jinsi ambavyo Serikali yetu haina mazingira mazuri ya uwekezaji. Zimekuwa ni ngonjera nyingi hapa na kukandamiza demokrasia na kupiga wapinzani na yote yanayoletwa hapa yanakuwa hayatekelezeki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niwaombe Wabunge, hii nchi ni yetu sote na wala hatuitaji kugombana, tunahitaji kama Wabunge tuongee lugha moja lakini kwenye ukweli tumwambie mtu amefanya vizuri na kama amefanya vibaya tumwambie amefanya vibaya. Msingi wa kwanza lazima turudishe demokrasia katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii hali mnayotaka kuiweka kwenye Chama cha Mapinduzi ya kuogopa watu mnaitoa wapi? Hata Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema tusiogope watu, tuwaheshimu watu. Leo ndani ya chama chenu mmeanza kuogopa watu hicho chama chenu hakina wazee cha kuwaonya watu wasiogopwe? Hivi vyeo ni dhamana, alikuwepo Baba yetu wa Taifa na nataka niwaambie Serikalli ya Awamu ya Tano msidhani wale wa Awamu za Kwanza, ya Pili, ya Tatu na ya Nne hawajafanya mazuri na hata wapinzani hatusemi hivyo, kuna mambo mazuri ambayo Baba wa Taifa aliyafanya lazima tuyaenzi na kuyaheshimu, lakini kuna mambo mabaya aliyoyafanya tutayakataa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi kuna mambo mazuri aliyafanya na mabaya aliyafanya mazuri tutayaheshimu na alikosolewa, alisikiliza, tukampenda. Akaja Mheshimiwa Benjamin William Mkapa alifanya mambo mazuri tukampigia makofi, tulipenda hata hotuba zake za kila mwisho wa mwezi zilikuwa ni hotuba zilizoshiba siyo za vijembe za kutukana watu, lakini kuna mambo mabaya tulimsema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, akaja mzee wetu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na kwamba tulim-challenge ni kweli, pamoja na kwamba kuna mambo hatukukubaliana naye lakini alisaidia nchi hii kwenda mbele. Kipindi chake aliweka mazingira walau watu duniani walianza kupenda kuja kuwekeza Tanzania na walau aliruhusu demokrasia. Tulimsema humu ndani lakini alihakikisha kila mtu kama Mtanzania anatoa mawazo yake, leo kwa nini Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli asisemwe? Tulikuwa tunakaa naye pale kwenye kiti tunamfuata pale leo tunamuogopa ana mapembe? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Wabunge wa CCM hebu tuweke itikadi zetu pembeni, tusimame kama Bunge, Rais akikosea tuwe na uwezo wa kusema no, wewe ni Rais wetu lakini hapa no. Hatuwezi tukawa waoga, anatisha kila mtu na kila mtu anajipendekeza kusema uongo. Hii nchi ina hali mbaya lazima tushirikiane. Ninyi mnaopeleka hiyo mipango kwa sababu mnamzingira akisimama kwenye vyombo vya habari anasema wale waliokuwa wanaiba pesa ndiyo wanapata taabu, hivi maskini wanaouza vitumbua kule…
T A A R I F A...
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya Mheshimiwa Simbachawene siipokei na haya ndiyo niliyoyasema ndiyo uoga tunaouzungumza huo. (Makofi)
La pili hayo maneno aliyoyazungumza Mheshimiwa Simbachawene wakaongee kwenye party caucus. Hapa tunaongea...
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ndugu zangu nimesema hapa hakuna mpinzani yeyote anayesema Serikali zilizopita hakuna mazuri yaliyofanyika, hakuna anayesema hivyo. Tunachosema mabaya tutakosoa na tutaendelea kukosoa. Kama ninyi mnamuogopa Mtukufu Rais sisi tutamsema, tutamkosoa ndani ya Bunge na nje ya Bunge na akifanya vizuri tutamwambia.
Niombe Wabunge wote tushikamane, tunapojadili mambo mazuri ya nchi wote tuwe pamoja uchumi uko vibaya, hakuna pesa mifukoni hakuna pesa kwa watu. Mheshimiiwa Rais mnam-mislead eti anasema waliokuwa wanapiga rushwa ndiyo wana shida huko mitaani mama ntilie kwenye majimbo yenu walikuwa wanapiga rushwa wapi?
Watu wana hali mbaya. Wanashindwa kulipiwa ada halafu mnakuja hapa mnasema wapiga rushwa walikuwa wanapiga rushwa wapi kwenye majimbo yenu. Hivi ninavyozungumza nyuso zenu zinawashuka kwa sababu mnajua ukweli huo kwamba hali ni mbaya. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba wote tuchangamke tumdhibiti Waziri wa Fedha alete mipango na bajeti inayoeleweka. Mawaziri wengine mnabeba mzigo sio wenu, wakati wa bajeti mwaka jana tulikuwa tukiwaambia pesa hazitoshi mnasema aah zinatosha hivyo hivyo. Sasa hivi kwenye Kamati mmerudi tena mnasema kwa kweli hazitoshi mtusaidie ninyi ninyi, sasa hivi mnasema hazitoshi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, suala tumbane Waziri wa Fedha alete mipango inayoeleweka siyo mipango ya ku-copy na ku-paste sijui kutoka wapi iwe katika mazingira ya kwetu. Tuletee mipango in our context siyo mme-copy New Zealand au sijui Australia huko it doesn’t work here.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.