Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo langu la kwanza, naomba nikumbushie siku nachangia bajeti hii ya Wizara ya Fedha nilisema tukikubali mipango hii ya Mheshimiwa Mpango, tutauza hadi Ikulu, tumeyaona leo hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge tumechangia, Mheshimiwa Waziri ametuelewa na hii ndiyo mara yake ya kwanza sasa hivi ana miezi minane tu. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge naomba tumpe nafasi, Waziri atajirekebisha. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili naomba nichangie masuala yanayoendelea sasa hivi kwa upande wa wafanyabiashara. Wafanyabiashara wetu sasa hivi hatuwapi nafasi, wanapotoa ushauri Serikalini, Serikali inawapa nafasi finyu ya kuwasikiliza. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba ukitoka hapa kakae na wafanyabiashara wetu. Mimi nina uhakika tukisikiliza maoni yao tutafika mbali. Haya yaliyotokea sasa hivi hayatatokea tena, ni masuala madogo tu ya kukaa na kuyarekebisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo langu la tatu, katika Jimbo langu la Ulanga kuna migodi mikubwa ambayo inatarajiwa ianze, kwa kiasi kikubwa italisaidia Taifa letu katika kuchangia uchumi. Hata hivyo, wananchi wa kule hawasikilizwi na kusababisha miradi hii kuchelewa kuanza ambapo ingechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa Taifa letu. Kwa hiyo, naomba Serikali, Mheshimiwa Waziri Mkuu upo naomba uje Ulanga utusikilize. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la nne, katika Wilaya yangu ya Ulanga tunalima mazao mengi ikiwemo mpunga zao ambalo kwa kiasi kikubwa linachangia uchumi wa Taifa letu. Leo hii Wizara ya Maliasili inapanga kwenda kuwanyang‟anya wananchi wa kule ardhi ambayo ingechangia kwa kiasi kikubwa mapato ya Wilaya ya Ulanga. Rais alipokuja aliahidi lile eneo watawaachia wananchi ili waweze kulima na kuchangia mapato ya Taifa hili.
Endapo tutawanyang‟anya wananchi eneo lile nakuhakikishia robo tatu ya mapato ya Ulanga na Malinyi yatashuka. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba suala hilo ulitazame katika jicho la pekee. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tano, jana kuna kiongozi mmoja alinishangaza sana, aliuliza Serikali ya CCM itatumia miujiza gani kutekeleza ahadi zake. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na wananchi wa Tanzania kuwa Serikali ya CCM haitumii miujiza inatekeleza ilani yake kwa mipango na mikakati na itafanikisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi namshangaa, kwanza ajiulize yeye huyo kiongozi form six amepata division zero, lakini huyo huyo ana miujiza ya kuwaongoza wanasheria maarufu kama akina Tundu Lissu wakatulia, ana uwezo wa kuongoza madaktari wenye Ph.D na wakatulia. Kwa hiyo, sisi hatutumii miujiza tunatumia taratibu, kanuni na uadilifu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la sita, kumekuwepo na sintofahamu Wakuu wetu wa Wilaya, Wakuu wetu wa Mikoa kutumia sheria ya kuwaweka ndani wafanyakazi wenzao kama Madiwani na watendaji wengine kama Wakurugenzi wa Halmashauri, kile kitendo cha kuwaweka saa 24. Wakuu wa Wilaya wametumia ile kama silaha yao ya kuwakandamiza viongozi kwa ajili ya kuwalipizia visasi. Kwa mfano, kila siku tunasikia Mkuu wa Wilaya amemweka ndani Mkurugenzi, kila siku Mkuu wa Wilaya amemweka ndani Diwani, vile vitu vinadhoofisha maendeleo ya nchi yetu. Watu wamekuwa hawafanyi kazi kwa juhudi zote, wanafanya kazi kwa uoga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu aliangalie hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie hapo.