Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Mapendekezo ya Mpango ambayo yamewasilishwa leo na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango. Nishukuru Mpango umeeleza mambo mengi na umejikita kwenye mambo mengi makubwa zaidi. Inawezekana yakawa size ya uwezo wetu kama nchi au yakawa zaidi ya uwezo wetu kama nchi kwa sababu projections zilizopo kwenye Mpango huu ni kubwa kiasi fulani.
Mimi nataka kujikita zaidi katika kutoa ushauri ushauri kuhusiana na mwelekeo mzima wa huu Mpango ulivyo na mbele tunakokwenda. Mchango wangu zaidi utajielekeza kwanza kwenye sekta ya kilimo, lakini na uanzishaji wa viwanda kwa bidhaa zinazotokana na kilimo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango huu ulitakiwa zaidi uoneshe mwelekeo sahihi kwenye kilimo na hasa kwenye uzalishaji ili tuweze kupata dira na mwelekeo wa kuelekea kwenye viwanda. Tunajua kwamba kutakujakuwa na udadavuaji wa baadhi ya mambo lakini kwa hivi ilivyoelezwa ndani ya huu Mpango iko too brief na hapa ndipo penye roho ya uchumi na maisha ya Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza katika hili, mpango haujaeleza mkakati mzima wa udhibiti na uendelezaji wa maeneo yale ambayo mazingira yake yameathirika. Miaka kumi iliyopita Tanzania ilikuwa zaidi inategemea mikoa minne kwa upatikanaji wa mvua ya uhakika, lakini sasa hivi hiyo mikoa minne tuliyokuwa tunasema ina mvua ya uhakika imeshapoteza mwelekeo. Tulikuwa tunaiangalia zaidi Kigoma, Kagera, Katavi, Njombe pamoja na Iringa. Hata hivyo, kwa kiasi kikubwa maeneo haya yamekumbwa na uharibifu wa mazingira na unapoweka mpango kama huu ambao unataka kutengeneza mazingira ya uzalishaji, vitu hivi lazima viwe na mtazamo maalum.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo yetu tumeyaharibu, tukiangalia eneo kubwa tulilokuwa tunalitegemea, tunaliita eneo chepe la mabonde ya Usangu mpaka Ruaha leo hii imekuwa ni mbuga ya kufugia ng‟ombe tu. Hata tukienda maeneo yale ya Kagera, Karagwe, Misenyi na Biharamulo nayo vilevile tumeyaachia huru as if nchi yetu haina mpango mkakati wa udhibiti wa uharibifu wa mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo langu, turudi kwenye kuweka mkakati maalum wa udhibiti wa uharibifu wa mazingira katika maeneo hayo ili kurudisha uoto wa asili na hali nzuri ya unyeshaji wa mvua katika maeneo yale. Sambamba na hilo, ule mkakati uliokuwa umeanzishwa Dar es Salaam wa upandaji miti, tunarudia tena, uweze kusambaa nchi nzima kuwe na mkakati kama ule vinginevyo hatma ya nchi hii ndani ya miaka kumi tutakuwa kwenye mtihani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo, ni lazima nchi iwe na mkakati wa kuhakikisha kwamba kunakuwa na uzalishaji. Kwa kipindi hiki sasa mkakati mkubwa uelekezwe kwenye umwagiliaji maji. Bado mpango haujaonesha kiwaziwazi mkakati wetu wa ujengaji ama mabwawa au miundombinu yoyote ya umwagiliaji maji kwa kutumia rasilimali ya mito na maziwa tuliyonayo hapa nchini. Tanzania tumejaliwa, lakini mpaka tunajiuliza sijui tumerogwa wapi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano tuliokuwa nao sisi wengine tuliopata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya nchi za wenzetu, mwezi uliokwisha kulikuwa na kikao cha wataalam wa kilimo cha SADC pale Angola, Wamisri walikuja kutoa taarifa na uzoefu wao tu, kwa kutumia maji ya Mto Nile, ile Suez Canal, wenyewe wanaita Suez Belt, wana uwezo wa kuzalisha pamba tani milioni tano kwa miaka miwili. Sisi tuna Ziwa Victoria lakini uzalishaji wetu kwa Kanda ya Ziwa ambayo ndiyo maarufu kwa ajili ya uzalishaji wa pamba tunasuasua kwenye tani 300,000, wenzetu wanazungumzia kuongeza kutoka milioni tano kwenda kwenye milioni nane sisi tunaangalia 300,000 tutai-maintain vipi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango huu ili uwe smart uangalie raw material zinazotokana na uzalishaji wa mazao mbalimbali ya kilimo. Hata hivyo, mwelekeo wetu uwe kwenye irrigation ili na sisi kama wananchi tupate fursa ya kutumia maji na mito ambayo ipo ndani ya maeneo yetu, kitu ambacho bado hakijatendeka vilivyo. Maji tunayo yanaishia baharini kama wengi walivyosema. Nikuombe Mheshimiwa Waziri tukafanye restructuring kwa baadhi ya mambo tuelekeze nguvu kwenye umwagiliaji maji ndipo tutakapokomboka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu nyingine ni usalama wa chakula, tuwe na mipango ambayo itatuwezesha kuwa na uhakika wa usalama wa chakula hapa nchini. Kwa kweli bado na mimi nasema ni aibu nchi hii kulalamika njaa wakati fursa za vyanzo vya maji tulivyonavyo ni nyingi sana lakini bado hatujajiweka sawa, mipango yetu haijajielekeza kuhakikisha kwamba watu hawa wanalima kwa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano mmoja, kama tutaweza kujenga mabwawa yakawa yanatumika kwa kilimo na mifugo, tukaweza kuendeleza hekta 50 tu kila Mkoa kwa yale maeneo yenye uwezekano wa kutengeneza yale mabwawa tuna uhakika wa reserve ya tani 500,000 kila mkoa kwa kila mwaka. Hii ni akiba nzuri lakini hiki ni chanzo cha raw material ya viwanda ambavyo tunategemea tuvianzishe na maeneo mengine yatumike kwa ajili ya chakula na mambo mengine. Tuwe na mkakati na muono wa mbele wa kuona kwamba nchi inakuwa na uhakika wa ile reserve iliyokuwa tunaisema tu lakini kuweka reserve ya chakula kwa kutegemea mvua ambazo hazina uhakika bado hatujaenda vizuri na hatujawa stable. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe sana Mheshimiwa Waziri tuzingatie kuyafanyia marekebisho baadhi ya mambo, mtuite tuwape mawazo ambayo yataweza kutujenga. Kinachotia uchungu ni kwamba tunatumika katika nchi za wenzetu kutoa mawazo ambayo wao wanayafanyia kazi na wanaweza kupiga hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kilichotokea mwezi uliokwisha, wenzetu wa Malawi baada ya kupata tatizo kubwa la ukame mtazamo wao sasa hivi ni huo. Haya maelezo ambayo mmeyatoa hapa katika page number 16 ya mpango tuliokuwa nayo ni mkakati ambao EU kwenye agricultural sector ndiyo waliokuwa nao, AU ndiyo waliokuwa nao na SADC wame-copy and paste huohuo.
Kwa hiyo na sisi tusiwe tunauweka kimaandishi, tuuweke kivitendo uwe practical na siyo tunachukua mipango kama hii na maelekezo ambayo wenzetu wameyaweka sisi kwetu baadaye yanaishia kwenye shelf. Nimuombe sana, tusipozingatia na tukaelekeza nguvu zetu kwenye kilimo tumewamaliza Watanzania na tutakuwa na ndoto tu ya viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mpango bado haujatuambia kwenye uvuvi tunafanya nini. Tumepata maelezo na baadhi ya watu wameeleza lakini katika eneo kubwa ambalo tutaweza kuajiri watu wengi kabisa ni sekta ya uvuvi. Tukijipanga vizuri katika eneo hili, wenzetu wametoa mawazo pale kwamba tutafute angalau meli moja tu ya uvuvi ina uwezo wa kutuanzishia viwanda viwili lakini ina uwezo wa kutoa ajira kwa watu mpaka 3,000. Kwa sababu kazi zilizopo kupitia sekta ya uvuvi ni nyingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tutengeneze mazingira ya pale bandarini kuwepo na port dock ambayo itawalazimisha wale wanaovua katika maeneo mengine yote ile kuchakata wale samaki na process nyingine zifanyike katika maeneo yetu, tutatengeneza pesa ya kutosha. Taarifa zilizopo sasa hivi duniani, Tanzania baada ya kuzuia leseni za uvuvi katika uvuvi wa bahari kuu, demand ya samaki katika soko la dunia imepanda mpaka tani 230,000, soko lipo wazi, nafasi hii ndiyo pekee ya kuitumia. Nimuombe Waziri wetu wa Kilimo azuie kutoa vibali vya uvuvi wa bahari kuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunaofuatilia haya mambo na tunayajua, ukiikodi meli moja ya uvuvi Philippines au Thailand wanakodi kati ya dola milioni tano mpaka milioni saba, catchment yake kwa wiki tatu mpaka miezi miwili ina thamani ya dola milioni 40.
Kwa hiyo, kwa wale wanaokodi, kwa wenzetu wanafanya deal kwamba akikodi meli mara moja harudi tena baharini kapata utajiri wa maisha anafanya mambo mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa utafiti unavyoonesha samaki wale wengi wanawatoa katika maeneo yetu na wakija katika maeneo yetu haya hawavui jodari tu peke yake, wanavua kamba, pweza, ngisi na samaki mbalimbali na baadaye wanakwenda kufanya uchambuzi katika maeneo yao sisi tunabaki kama tulivyo. Ile ni bahati, ni riziki Mungu katupa tujipange vizuri tuitumie vizuri ilete manufaa katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo linajieleza hapo, tutakapoweza kuwa na eneo la kuweza kushusha samaki, tukaweza kuanzisha maeneo ya majenereta ya kuhifadhia vizuri samaki, tutaweza kuongeza ajira kubwa kwa sababu wenzetu Ulaya wanachotaka ni minofu. Hivi sasa biashara kubwa iliyojitokeza maeneo ya Kongo ambao wanakuja kuchukua dagaa kwa wingi sana Zanzibar, Mwanza na Kigoma wanakwenda kutengeneza raw material ambayo wanapeleka Ulaya kama ni fish meal, demand yake sasa hivi ndani ya soko la dunia kubwa. Sisi tukiwa na meli hiyo pale zile by products zilizotokana na kutoa zile nyama za samaki tunatengeneza fish meal kwa kiwango kikubwa sana ambapo soko ndani ya eneo la soko la dunia ni kubwa sana. Fursa nyingine ni hizo, pale hutupi kitu, hata ule mwiba wa katikati wa samaki bado ni bidhaa adimu kabisa kwa sababu ile calcium iliyomo mle ni bora zaidi na inahitajika katika maeneo mengi sana kwa ajili ya kutengeneza bidhaa mbalimbali na dawa.
Kwa hiyo, mimi wito wangu na wazo langu ni kuiambia Serikali hili eneo la uvuvi lina fursa kubwa sana, kuliko kuwaita Wachina kuja kuweka soko pale la bidhaa zao mbalimbali, hapa pana pesa za waziwazi, tujikite jamani katika maeneo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ninalotaka kuzungumza ni kwenye mazao ya biashara bado kama nchi tunaendekeza ukiritimba fulani hivi ambao hauleti maana. Leo hii kutengeneza rustan coffee mpaka twende Moshi, Arusha? Gharama za kuchukua kahawa iliyoko Mbinga ambapo kule tunafanya process ya mwanzo tu ya catchment uisafirishe uipeleke Moshi ni kubwa. Wakati mwingine unachukua kahawa kutoka Manyovu au Kigoma iende Moshi, very unfair! Tutengeneze viwanda ambavyo tutaweza kutengeneza kahawa ambayo itaweza kwenda kuuzwa katika soko la nje moja kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kahawa yetu ni ya nne duniani, bado tuna nafasi kubwa. Kwa ubora hatujawapita Ethiopia, Rwanda lakini tumewapita Uganda, Burundi na Kenya. Kahawa yetu ni bora kuliko ya Brazil, bado tuna nafasi katika soko la dunia. Hata hivyo, utaratibu wa makampuni yanayoshughulika na zao la kahawa ni wa kujitengenezea faida wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi hiyohiyo ipo kwenye tumbaku. Tumbaku kilichotokea pale ni ukiritimba tu wa yale makampuni ya kujifanya wao ndiyo wao wakati bado kuna fursa kubwa ya ile tumbaku katika soko la dunia. Mnunuzi mkubwa wa tumbaku ni China. Sasa hivi China baada ya kuona bureaucracy ya Afrika anatenga hekta karibu milioni mbili azalishe tumbaku nchini mwake, lakini mbegu ya tumbaku kutoka China sisi tunayo hapa. Sasa lile tishio la yale makampuni la kusema kwamba sisi hatununui wanasema wanatisha bwege ni ili sisi tuweze kujiachia hawanunui tupunguze uzalishaji ili wao …
MWENYEKITI: Ahsante.