Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nikushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia mpango huu ambao umeletwa mbele yetu. Mpango huu ni mzuri sana, una mwelekeo mzuri na dira nzuri ya kuhakikisha shughuli zote ambazo zimepangwa hapa zinakwenda vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua hata vitabu vitakatifu vinasema unapotaka kwenda peponi au mbinguni ni lazima ukeshe ukiomba. Sasa kazi ya kukesha na kuomba si ndogo, ni kubwa sana, kazi ya kukesha na kuomba na ukishakesha na kuomba ndio unaweza kufika peponi au mbinguni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya Awamu ya Tano kazi kubwa ambayo ilikuwa ikiifanya ni kuturudisha kwenye mfumo, kuachana na ule utaratibu tuliouzoea kwa hiyo, ilikuwa inaturudisha kwenye mfumo. Turudi tujenge nidhamu katika Serikali na kazi hiyo imefanywa na Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amefanya kazi nzuri sana. Hata wakati anawaambia Watanzania anaomba ridhaa aliyasema haya kwamba, nipeni nitafanya moja, mbili, tatu; leo anayafanya haya tunasema aahhaa, anafanya vibaya! Lakini mtu mmoja amewahi kusema ukiona mtu anakusifia jiangalie mara mbili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi inayofanywa na Serikali kupitia Mawaziri waliopo na huyu ambaye ameleta mpango huu ni kazi nzuri sana. Sasa kwamba Serikali imeturudisha kwenye mfumo, imedhibiti mambo ya pesa, Mheshimiwa Mpango baada ya kudhibiti sasa peleka kwenye Halmashauri ili zikafanye kazi, maana kwanza alikuwa anaturidisha kwenye mfumo na sasa tumerudi kwenye mfumo, kwa hiyo fedha sasa zianze kwenda kwenye Halmashauri ili zikafanye kazi iliyokusudiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane na wenzangu waliozungumzia habari ya Liganga na Mchuchuma. Na mimi napata ukakasi, hivi kuna tatizo gani linalofanya shughuli ya Liganga na Mchuchuma ikwame? Kwenye mpango imekaa vizuri, tunaomba Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana suala la Liganga na Mchuchuma hebu sasa liweze kusonga mbele kadri ambavyo lilikuwa limepangwa ili liweze kusaidia Tanzania, tuweze kupata ajira nyingi kwa vijana wetu wa Tanzania kama ambavyo mpango upo vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua napata taabu kitu kimoja kidogo sana! Mambo mengi amenimalizia yuko pale, ambayo nilikuwa nimeyaweka hapa kwa sababu...! Sasa naomba niseme! Eeh, ndio mwenyewe! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, humu ndani wote ni Wabunge sawa, kila mmoja ana hadhi yake ameingia hapa, tunahitaji kuheshimiana. Tunapomnyooshea mtu, Mbunge mwenzako kwamba eti wewe huoni uchungu kwa sababu uliteuliwa, tena huyu ndiye anaheshima kubwa sana kuliko wewe, kwa sababu kama alivyosema Mbunge mwenzangu pale kwamba kila mmoja amepata kura kwa idadi tofauti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nani aliyepata humu ndani kura nyingi kama za Mheshimiwa Magufuli, nani? Sasa zile zote si ndio amepewa yule kwa heshima ya Watanzania? Ndugu zangu tuheshimiane, aliyeteuliwa, ambaye hakuteuliwa wote ni Wabunge. Wakati fulani ninyi wenyewe ndio mnatoka huko mnakwenda pale, Waziri eeh, moja, mbili, tatu! Ni Waziri huyu, apewe heshima yake kama ambavyo Wabunge wengine tuko hapa ndani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa baada ya kudhibiti mambo yote sasa peleka fedha Halmashauri zikalipe na fidia zile pamoja na Makambako ikiwemo. Kuna fidia kule wananchi wangu wanadai kule ili zikaweze kufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ujumla mpango huu nauunga mkono vizuri, ni mpango mzuri ambao sasa peleka fedha zikaanze kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sina la ziada. Ahsante sana.