Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuchangia. Jambo la kwanza, ningependa kumwomba Waziri wa Fedha asirudie aliyoyafanya wakati analeta Mpango wa Mwaka 2016/2017. Tutakayomshauri a-take into consideration kwa sababu hii nchi ni yetu sote. Nchi hii siyo ya executive only, ni nchi yetu sote Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nataka nishauri, ndugu zangu wa UKAWA, nimesoma hotuba aliyoisoma dada yetu Mheshimiwa Halima, kuna a lot of constructive issues. Hii nchi ni yetu sote, mkisema viwanda kizungumkuti kwa maana ya zile abusive language mnatufanya na sisi tuwe defensive na kusahau content mliyoweka ambayo ina substance kwenye maendeleo ya nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii iki-develop wote tuna-develop. Kuna mambo mengine mnasema ni ya msingi sana lakini inatufanya tu-defend kwa sababu ya lugha inayotumika. Nimemwambia nje na nasema humu ndani ili iingie kwenye rekodi. Linapokuja suala la Mpango wa nchi tuweke siasa pembeni tujadili Mpango wa nchi. Waziri wa Fedha asipochukua yale tunayoamini ni kwa maslahi ya nchi yetu na watu wetu tuna jukumu la kuungana bila kuangalia vyama vyetu, hili ni jambo la pili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nianze kwa masikitiko, premises alizoziweka Waziri wa Fedha kwa ajili ya msingi wa bajeti anayokuja nayo ni premises ambazo zinatujengea failure. Ukienda ukurasa wa 14, item 2.3.10, ametaja item kama saba ambazo ndiyo msingi wa Mpango na bajeti ya 2017/2018, hii ndiyo pillar. Item ya mwisho anasema, kuwepo kwa sheria na taratibu wezeshi kwa uwekezaji. Ukiangalia taarifa ya Kamati, World Bank Report inatu-rank ni wa 139, doing business in Tanzania is very difficult. Ni jukumu lake Mheshimiwa Waziri akaangalie sheria za nchi hii kama zina-attract investment?
Mheshimiwa Mwenyekiti, item number five anasema, hali ya hewa ya nchi na katika nchi jirani ni nzuri, which is not right! Hali ya hewa ya nchi kwa mwaka 2017/2018 tuna-project kuwepo kwa ukame. Nchi zilizotuzunguka zina hali mbaya ya chakula, taarifa ya TMA inaonesha kwamba kutakuwa na ukame, yeye anasema itakuwa nzuri, we are failing! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, anaendelea kusema, kuendelea kuimarika na kutengemaa kwa uchumi wa dunia, Mheshimiwa Waziri anatoa wapi hii fact? Global trade imeteremka by 0.08! Siyo maneno yangu, ni ya World Bank, ni ya IMF yanaonesha na uki-google report ya World Bank ya tarehe 20 Oktoba, 2016 inasema wazi kwamba bei ya mafuta duniani inapanda, Waziri anasema itaimarika. Tulivyopitisha bajeti iliyopita na bajeti hii mafuta yamepanda kwa zaidi ya dollar 10! Kaka yangu anasema unaimarika, this is very bad! Hii nchi ni yetu sote, tulisema kwenye mpango wa mwezi Februari, tukasema sana kwenye bajeti, yale yote tuliyomshauri humu ndani akaja akatuona humu ndani Wabunge wote hatuna akili, leo tunaathirika kama nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ripoti hii ya Waziri ya Mapendekezo ya Mpango inazungumzia growth ya biashara yetu ya nje by 7.4, very good! Kataja mazao, katani, tumbaku na nyuzi, nimechukua hii document, nimeangalia kwenye agro sector, hakuna sehemu anapanga kuongeza uzalishaji na ku-invest kwenye hizi bidhaa ambazo zimetuingizia fedha, what is this? Anachosema huku na Mpango wake havifanani! Kaka sisi Chama cha Mapinduzi tumewaahidi wananchi, au kwa sababu kaka yangu hajaenda kuomba kura? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, CEO wa Nokia wakati imekuwa taken na Microsoft alisema, we did not do anything wrong but somehow we lost, sisi tuko excited na historical fact, the world is changing! Tusipobadilika we are going to perish. Soma Mipango, Liganga na Mchuchuma mimi sijaja Bungeni naisikia, iko chini ya NDC, hebu jiulizeni kwenye Mipango, NDC toka lini inapelekewa fedha na nchi hii na mnitajie subsidiary moja iliyo-succeed NDC, nothing! Hakuna subsidiary iliyo succeed! Nashindwa kuelewa what are we thinking? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri anazungumzia, Mungu huyu! Waziri anazungumzia 32, 33 trillion shilling budget, area ya kwanza ni makusanyo ya kodi kuongezeka kwa 16%, maana yake tuna mpango wa kwenda kuongeza kodi na mzigo kwa wananchi by 16%. Tuliwaambia msiweke kodi kwenye money transfer hamkutusikiliza, tuliwaambia msiweke kodi kwenye tourism hamkutusikiliza, tuliwaambia msiweke kodi kwenye maeneo mengi, mnajua matokeo yake? Quarter iliyopita commercial banks zimeshuka profitability by 94%. Implication yake ni moja, income tax itakuwa chini, excise duty zitaporomoka, there is no hope!
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini ninachotaka kushauri? Moja, Dkt. Mpango kaka yangu, I respect your academic background; kodi should not be your target kwenye kila jambo. Haina maana kuweka kodi kwenye kila kitu, kwenye maeneo yale yale we are killing the business. Tutumie strategic location ya nchi, nataka nitoe mfano mdogo, it’s not a rocket science, Dubai ime-grow because of airport, tuna best location hapa lakini one of the expensive landing katika dunia hii ni Tanzania, futeni kodi kwenye viwanja vya ndege, fanyeni this is the hub, we will grow! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mnaleta issue ya Kurasini kutengeneza gulio la Wachina mnaua Kariakoo. Maana yake Wachina waje pale waweke bidhaa zao halafu iwe ni free tax kuziweka pale halafu ikitoka ndiyo tuchukue kodi, hatuna hizo control mechanism! If you want to establish a free market with zero tax fungueni soko la Kariakoo waacheni Waswahili wale wauze pale ikitoka tukusanye kodi! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tumekuwa wakusanya ushuru wa Kongo…
(Hapa kengele ya kwanza ililia)
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Muda umekwisha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna uwezo wa kutengeneza fedha sana, alisema kaka yangu kwenye Bunge lililopita, Mbunge wa Kahama tuanzisheni soko la madini, yeyote atakayeleta madini yake hapa Tanzania aingize bure, yakiuzwa yakitoka tutapata kodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea kuhusu agro sector. Nataka niwaambie, tunazungumzia kwamba tunataka kuondoa umaskini, kama hatufikiri sawasawa kwenye kuwekeza zaidi kwenye sekta za kilimo na uwekezaji wetu wa viwanda ukagusa maeneo ya kilimo there is no way tutapambana na umaskini wa nchi hii. Hapa nimesikia Wabunge wanalalamika dawa hamna, Wabunge wanalalamika kuhusu mikopo, nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, mimi natoka Kamati ya Huduma za Jamii, Kamati ya Guantanamo, ndiyo inayosimamia Sekta ya Elimu na Afya, mtamtoa roho Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla bure, mtamtoa roho Mheshimiwa Ummy, mtamtoa roho Mheshimiwa Profesa Ndalichako, MSD, if we will not rectify our economy hatuwezi kuondoa matatizo ya afya. Sasa kama Wabunge tunataka kweli kusaidia Serikali tu-deal na Wizara ya Fedha. That is the only solution!
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Waziri wa Fedha ha-cherish private sector, wanasheria wanajua kuna kitu kinaitwa law of negligence, huwezi kwenda Kariakoo umeshika burungutu la shilingi milioni 10 unatembea halafu watu wakichukua ulalamike. Tuliacha milango yetu wazi muda mrefu, wafanyabiashara wakatumia opportunity, wakavuta, leo kwa uzembe wetu uliowa-attract wao kukwepa kodi na wizi mwingine ulikuwa masterminded from the Government, it is true!
This is the naked truth. Kwa nini mpaka leo mindset ya Serikali na Wizara ya Fedha ni kwamba business community ni wezi? No one will come to our market. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwape mfano mwingine, Waziri anasema uchumi umekua kwa asilimia 6.7 katika kipindi cha miezi sita ya kwanza na moja ya eneo ambalo limechangia kukua huko ni minerals. Mimi najiuliza sana na nashangaa taarifa zake, najiuliza kuna tatizo Serikalini? Production ya Tanzanite imeshuka by 50% toka tumewauzia wale wahuni ule mgodi, hiyo growth inatoka wapi? Tunasema fedha imekua, imekua kutoka wapi wakati wana-register losses, private sector can not access loans from the financial institution na siyo kwa sababu hawana hela ni kwa sababu hakuna security sokoni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo biashara zina-collapse nchi hii, leo mabenki yanapata hasara. Nataka niitahadharishe Serikali, if we will not be careful na Waziri wa Fedha usipofanya intervention kwenye financial institution, real estate is going down na wengi waliokopa watashindwa kulipa, tutaingia kwenye matatizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.