Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii ambayo nimeipata kuingia kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Niwashukuru sana wapigakura wangu wa Jimbo la Kasulu Vijijini kwa kura nyingi sana ambazo wamenipa na kunipa Halmashauri yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo nimpongeze sana Mheshimiwa Magufuli kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi sana kuwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, lakini na Baraza lake lote ambalo leo hii linachapa kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu mimi pamoja na Watanzania wengi tunayo imani kubwa sana pamoja na kasi ambayo mmeanza nayo. Chapeni kazi, longolongo, umbea, majungu, achaneni nayo, fungeni masikio angalieni mbele, pigeni kazi. Mwanafalsafa mmoja aliwahi kusema kwamba; “you cannot carry fundamental changes without certain amount of madness.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo niseme tu, nimepata nafasi ya kusikiliza michango mingi sana pande zote mbili katika kuboresha kitu hiki. Nimewasikiliza Wapinzani, lakini nimeguswa sana sana aliposimama kuchangia Mheshimiwa Lema. Mheshimiwa Lema ameongea vitu vingi sana hapa ambavyo kimsingi vimenigusa, lakini kwa sauti yake ya upole ya kutafuta huruma ya wananchi, imedhihirisha kwamba, yale Maandiko Matakatifu yanayosema kwamba angalieni watakuja mbwa mwitu wakiwa wamevaa ngozi ya kondoo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme, Mheshimiwa Lema amesema sana kuhusu demokrasia. Anadai kwamba Chama cha Mapinduzi kinakandamiza sana demokrasia katika nchi hii, lakini tukumbuke chama chake, mgombea wao Urais mazingira ambayo walimpata, kahamia kwenye chama chake, kesho yake akapewa kugombea Urais, hiyo ndio demokrasia! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwenyekiti wa Chama chao ni yule yule na wakati wa uchaguzi wale wote waliotangaza ndiyo wagombea Uenyekiti walifukuzwa kwanza na uchaguzi ukafanyika je, hiyo ndio demokrasia?
Pia kuhusu Viti Maalum, hakuna chama ambacho kimelalamikiwa katika nchi hii kama Chama cha CHADEMA katika mchakato wa kupata Wabunge wa Viti Maalum hiyo ndiyo demokrasia? Mnataka demokrasia tufuate maslahi ya CHADEMA, hiyo ndiyo demokrasia ambayo mnataka tuje kwenu!
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niendelee kusema tu, wakati Lema anasema alimwambia Mwenyekiti atulie na ninyi nawaambia tulieni mnyolewe.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lema amezungumza kuhusu ugaidi hapa. Naomba nisema ugaidi ni inborn issue ni issue ambayo mtu anazaliwa nayo na sifa zake ni uhalifu na kila mtu anafahamu historia ya Lema hapa. (Makofi)
MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Anasema kwamba, anasema, tulia unyolewe tulia, tulia unyolewe vizuri, tulia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa....
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wamesema watu hawa kama nchi hii itakuwa na vurugu basi mapato au uchumi wa nchi hii utashuka, lakini kila mtu anafahamu kwamba Arusha ni Mji ambao ulisifika kwa kuwa na amani sana, Arusha ni Mji ambao ulisifika kwa kuwa na uchumi wa hali ya juu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii hapa Mjumbe yule aliyesimama amesema uchumi wa Arusha umeshuka. Leo hii kila Mtanzania anajua kwamba Mheshimiwa Mbunge aliyeko sasa hivi wa Arusha Mjini amekuwa ni chanzo cha kuchafua amani ya Mji wa Arusha na amesababisha uchumi wa Arusha kuporoka kwa kiasi kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wanataka twende kwao tukajifunze nini hawa! Tulieni mnyolewe vizuri. Lakini naomba niseme, ndugu zangu lazima tuwe makini sana na niwasihi, Wapinzani ni marafiki zangu sana wengi. Lazima tuwe wakweli na tulitangulize Taifa letu mbele.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Tunapoomba kuchangia, tuchangie katika namna ya kujenga, siyo katika namna ya kubomoa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu Mpango huu, mpango huu.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa baada ya kuzungumza hayo, niende kuzungumza yale ya wananchi wangu wa Jimbo la Kasulu Vijijini, dose imeshaingia hiyo.
Suala la kwanza, kwanza niungane na mchangiaji Mheshimiwa Zitto Kabwe kwa alichozungumza hapa, alizungumza kwamba, Kigoma ni miongoni mwa mikoa ambayo imeachwa nyuma sana. Pamoja na Mpango mzuri ule, naomba niseme kwamba kwanza kwa suala la miundombinu, iko barabara ya kutoka Nyakanazi mpaka Kidahwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wote wa Mkoa wa Kigoma wote wanafahamu kwamba hapo ndipo uchumi wa Kigoma umefungwa. Naomba sana Serikali ya Awamu ya Tano, niseme tu kwamba bajeti ijayo kama haitakuwa na barabara hii nitatoa shilingi kwenye bajeti hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, ni kuhusu reli ya kati kwa standard gauge. Reli ya kati ni mhimili wa uchumi wa nchi nzima ya Tanzania, lakini waathirika wakubwa sana ni sisi watu wa kanda ya magharibi. Naomba niseme tu, niungane na wachangiaji wote, tuhakikishe reli hii ya kati inajengwa kwa standard gauge. Narudia maneno yale yale, kama kwenye bajeti tutakapokutana hapa kuja kujadili maendeleo haya, reli hii kama hamjatuletea kwa kinagaubaga tutaijengaje kwa kweli nitatoa shilingi. (Makofi)
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine...
MWENYEKTI: Ahsante sana.
MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono. Ahsante sana.