Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Na mimi napongeza sana hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha, vilevile nataka niishukuru Serikali kwa mara ya kwanza kwa, tangu Wilaya yangu ya Ileje ianzishwe mwaka huu tumetengewa fedha kwa ajili ya barabara kwa kiwango cha lami kutoka Isongole kwenda Mpemba. Napenda kuishukuru sana Serikali kwa jambo hili na kwa kweli, wananchi wa Ileje wanaingojea hii barabara kwa hamu sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nizungumzie suala zima la vipaumbele vyetu. Tumesema kuwa tunataka kuboresha kilimo na kimewekwa kabisa katika mpango mkakati wa kuendesha kilimo wa SAGCOT, lakini nasikitika kuwa inapokuja katika kupanga bajeti kilimo hakijapewa ile bajeti ambayo ingestahili kuhakikisha kuwa wananchi wengi ambao ndiyo wamegubikwa na umaskini wangeweza kunufaika kwa kuhakikisha kuwa fedha nyingi inakwenda katika kuhamasisha kilimo bora, ufugaji na uvuvi, ili wananchi wale ambao ndiyo maskini wangeweza kusaidiwa na mpango huu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sisemi kuwa miundombinu na sehemu nyingine ambazo fedha hizi zimepelekwa hakuhitajiki, vilevile lazima tuangalie sasa hivi nchi yetu bado ni maskini kwa sababu, wananchi wengi hawajaguswa na ukuaji wa uchumi ambao tumeupata, na njia moja kubwa ilikuwa ni kupeleka fedha nyingi katika sekta zile ambazo zinagusa wananchi moja kwa moja na mojawapo ndio hiyo kilimo, ufugaji na uvuvi.
Kwa hiyo, tungependa sana Serikali inapojielekeza katika Mpango wa Maendeleo huko tunakokwenda ihakikishe kuwa zile sekta ambazo ndiyo zinazogusa wananchi na zikawainua kiuchumi ndio zinapewa kipaumbele katika bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kurukia kidogo kwenye masuala ya utalii. Utalii ni sekta muhimu sana katika uchumi wetu na ni sekta ambayo ikisimamiwa vizuri italikomboa hili Taifa, lakini nasikitika kuwa bado kwenye masuala ya utalii hatujatoa vipaumbele vinavyostahili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeona kuwa tumeweka kodi, tumeweka tozo mbalimbali ambazo moja kwa moja hizo zitaongeza gharama za utalii kwenye nchi yetu. Sasa hili wenzetu nchi jirani wameliona na wameziondoa, itabidi katika kuhakikisha kuwa tuna-harmonise hizi kodi za Afrika Mashariki tunaondoa hizo tozo ili kuhamasisha utalii mkubwa zaidi kuja Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la utangazaji wa utalii ni suala ambalo limepigiwa kelele sana humu ndani na Waheshimiwa Wabunge wengi na kwa kweli tunatia aibu kama Taifa. Bado hatujalipa umuhimu suala zima la kutangaza utalii wetu wa ndani pamoja na hata kwa wananchi wa nje. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa sana kusisitiza kuwa Serikali itenge fedha ya kutosha katika kuhakikisha kuwa utalii wetu unatangazwa...
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana.