Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikirejea maneno ya Wanasheria wanasema kwamba, mara nyingi haki yako inapoishia ndipo haki ya mwenzio inapoanzia. Tunapoangalia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 18(a) inatuambia kwamba, kila Mbunge ana haki ya kutoa mawazo yake hapa Bungeni, lakini pia, haki hii inaenda sambamba na wajibu. Ukiangalia Kanuni ya 74(4) na (6) ya Sheria ya Haki na Kinga na Maadili ya Bunge utaona pale kwamba, kila Mbunge basi anapaswa kuheshimu Kiti cha Spika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo ninasikitika sana nimekuja hapa ninauliza kulikoni. Inakuwaje leo naambiwa kuna Chama cha Demokrasia na Maendeleo, lakini demokrasia hiyo basi Majimbo haya yote yanawekwa mfukoni kwa mtu mmoja na leo tunahubiri habari ya demokrasia. Hili suala tumesema hapana. Leo tumefika mahali ambapo mhimili wa Bunge unakosa heshima. Ifike mahali tuseme mwisho na hatutaki kuona haya. Kiti cha Spika hakihitaji mwanasiasa, Kiti cha Spika kinahitaji weledi, mwanazuoni anayejitambua. Kiti cha Spika kinahitaji guru wa sheria; kwa hiyo, ninaomba hawa wenzangu ambao leo wako mitaani ambapo wametoka nyumbani kwa ridhaa za waume zao na wengine wametoka nyumbani kwa ridhaa za wake zao wafike mahali waone hili siyo mahali pake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijielekeze sasa moja kwa moja kwenye hoja yangu ya msingi. Leo ninapenda pia kumpongeza Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango kwa kazi yake nzuri, pamoja na yote tumeona kabisa suala zima la maendeleo tumetenga asilimia 40, leo ninapoongea hapa ninapata mashaka kwenye hili, tunapopeleka fungu hili lote kubwa kwenye masuala mazima ya maendeleo wakati sera na mipango ya nchi haziko nkwa ajili ya kumlinda mzawa hii ni hatari sana kwa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo nimesoma ukiangalia kwenye hotuba ya Waziri Mkuu page ya 24 utaona pale inatueleza kwamba kupitia Sheria ya Ajira na Wageni Namba 1 ya mwaka 2005 ambapo utekelezaji wake ulianza Septemba, 2015 Serikali waliweza kujipatia mapato ya takribani shilingi bilioni 21.01 lakini mbona mimi nafika kuona kwamba, hapa hapana. Hatuwezi kujivunia vyanzo hivi ambavyo vinakiuka taratibu na misingi ya ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninasema haya kwa sababu katika mchakato huu au katika Wizara hii tumeona Serikali pale imetuambia kwamba mnamo miezi sita kuanzia mwezi Septemba mpaka mwezi Machi mwaka huu Serikali iliweza kuridhia vibali vya wageni 779 ambao walikuwa hawana vibali vya kuishi nchini wala vibali vya kufanya kazi nchini Tanzania. Wizara iliridhia na watu hawa wakaingizwa kwenye ajira rasmi, wakapokonywa vijana wetu ajira na wakaingia mitaani. Leo tunaona Wachina wamekuwa mamalishe kule, Wachina wanauza mitumba, ajira ya kijana Mtanzania hailindwi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninafikiri vyanzo viko vingi, wenzangu wameongelea kuhusu utalii na maliasili; ninapenda kusemea suala la Wizara ya Maliasili. Ukiangalia bajeti ya Kenya mwaka jana ilitenga shilingi bilioni 84, wakati huo bajeti ya maliasili ya nchi ya Tanzania kwa mwaka jana ilitenga shilingi bilioni 6.2 kwa ajili ya ku-promote maliasili yetu Tanzania, katika kutengewa kule tuliona kwamba ni shilingi bilioni mbili tu ndio ilienda kwenye matumizi! Nikiwa Westminster University nasoma nilipata kualikwa kwenye moja ya kongamano ambapo hawa Bodi ya Utalii walikuja nchini Uingereza kutangaza maliasili.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilisikitika sana, nilienda pale nikakuta kwamba wenzangu Watanzania, wakati Wakenya wameleta pale chui, wameleta simba, Watanzania wamebaki kugawa business card. Watanzania wamebaki kugawa kalenda, ni vitu vya kusikitisha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niliambatana juzi na Mheshimiwa Nape Nnauye, Waziri mwenye dhamana ya Habari na Michezo tulienda pale Kilimanjaro. Inasikitisha sana, kile kivutio cha Mlima wa Kilimanjaro tulienda pale kukimbia Mbio za Marathon za ku-promote maliasili ya Tanzania, lakini cha kusikitisha tumeenda tumevalishwa t-shirt inasema; Mbio Zetu Bia Yetu yaani bia ya Kilimanjaro! Hiki ni nini?(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani, tunahitaji maliasili Tanzania…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ester, muda wako umekwisha!