Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Udhibiti wa Matumizi ya Dawa na Mbinu za Kuongeza Nguvu Michezoni

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Udhibiti wa Matumizi ya Dawa na Mbinu za Kuongeza Nguvu Michezoni

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, WASANII NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia katika hoja yetu hii ya Azimio la Mkataba wa Kudhibiti Matumizi ya Dawa na Mbinu Haramu katika Michezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kukupongeza kwa kazi nzuri ambayo unaifanya, kwa kuliendesha Bunge kwa kutumia Kanuni vizuri. Vilevile niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge ambao wamechangia katika hoja yetu hii na nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa jinsi alivyowasilisha hoja kwa umahiri mkubwa. Hongera sana Mheshimiwa Waziri wangu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na faida kubwa ambazo ziko katika mkataba huu tunaona hakuna vipengele vyovyote ambavyo hatuhitaji kuviridhia, kwamba hakuna reservations. Kwa hiyo ni mkataba mzuri, hii inaonesha wazi kabisa huu ni mkataba mzuri na ndiyo maana hakuna reservations zozote.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianzie tu na hili la kijana wetu huyu aliyepatwa na dalili, hakukutwa moja kwa moja na madawa lakini kulikuwepo na dalili ambazo zinaashiria kwamba kulikuwa na dawa za kuongeza nguvu kule Brazil, akafungiwa kwa miaka miwili. Sasa kutokana na hilo inaonekana kwamba mwaka 2015/2016 zimechukuliwa sample 14 na kupelekwa katika Maabara za Kimataifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati nzuri tunashukuru sana Wizara inafurahi na ina faraja kwamba sampuli zote hizi 14 hakuna hata moja ambayo ilikutwa na dalili za kuwepo na matumizi ya dawa au mbinu za kuongeza nguvu michezoni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mkataba huu una manufaa makubwa, mojawapo ni lile la kutoa elimu pamoja na mafunzo kwa vijana wanamichezo wetu pamoja na watalaam wengine, lakini pia inatoa fursa kubwa sana za utafiti. Nami nichukue fursa hii sasa kutoa wito kuwaomba watafiti wetu wajiandae, pale ambapo mkataba huu utakapokuwa umeanza kufanyakazi kuna maeneo mengi sana ya kufanyia utafiti na yanaelezwa katika vifungu mbalimbali vya mkataba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, wanaweza wakafanya utafiti katika maeneo ya saikolojia, maeneo ya utu wa wanamichezo, physiology, wanaweza wakafanya pia utafiti katika sayansi ya michezo, wanaweza pia wakafanya utafiti katika vitu mbalimbali ambavyo vinajitokeza kulingana na maendeleo ya kiteknolojia, kuna vitu vipya ambavyo vinaweza vikajitokeza kama matumizi au dawa za kuongeza nguvu. Kwa hiyo watafiti wetu wajiandae kufanya kazi katika maeneo haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna hoja moja ambayo imejitokeza kutoka kwa Mheshimiwa Hafidh Ali alipokuwa akichangia kwamba ni vizuri sasa tukafanya maandalizi. Nafurahi kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba Wizara imeshaanza kufanya maandalizi machache. Kwa mfano, kuna wataalam ambao tayari wameshaanza kupewa elimu ya awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumeshaandaa eneo pale katika uwanja wa Taifa kwa ajili ya ofisi ya National Anti-doping Agency. Kwa hiyo, maandalizi kama hayo yamefanyika. Pia yanatakiwa maandalizi ya kisera, kisheria na kanuni ambavyo napenda kulitaarifu Bunge lako kwamba Wizara yetu imejipanga vizuri kabisa kwa ajili ya hili, kuandaa, kurekebisha sera na kufanya marekebisho, kuipitia upya pia sheria yetu ya michezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Hafidh Ali pia katika mchango wake aligusia jambo ambalo naona pia ni muhimu sasa watafiti tutawaomba wajiandae kulifanyia kazi, kwamba kuna watu ambao unaona kabisa umri umepita lakini wanacheza vizuri tu mpira na amekuwa na mashaka kwamba labda kuna vitu wanavyotumia. Kwa hiyo, hili ni eneo ambalo pia watafiti wanaweza wakalifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna hoja nyingine ambayo inahusiana na matumizi ya bangi na pombe katika michezo. Suala la pombe lipo limezuiliwa na liko katika kundi la alcohol, lakini kuzuiwa kwake ni wakati wa mashindano tu. Kwa hiyo hili nalo tutaliangalia, wakati wa kutunga sheria nitaomba Bunge lako pia liangalie kama kweli izuiliwe kwa wanamichezo wakati wa mashindano tu au sasa watazuiwa moja kwa moja sijui, lakini bangi inazuiwa na iko katika kundi la cannabinoids. Bangi inazuiwa kabisa, hairuhusiwi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna hoja nyingine ambayo ameichangia Dkt. Ndugulile kwamba, hata zile dawa ambazo ni za tiba zinazuiliwa. Naomba kumtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, kipo Kifungu cha 34 katika Mkataba huu na hiki Kifungu kinaruhusu sasa ile World Anti-Doping Agency, kufanya Amendments kwa ile list ambayo ni prohibited list ili therapeutic use exemptions. Kwa hiyo utaona kwamba, hii WADA ikifanya amendments masuala ya dawa kwa ajili ya matumizi ya kiafya yanaweza yakaruhusiwa kutumika.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru tena kwa kunipa nafasi na naunga mkono hoja. Ahsante sana!