Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kama ilivyowasilishwa hapo mbele. Miaka ya hivi karibuni Tanzania imewahi kuingia kwenye mgogoro na nchi jirani ya Malawi kuhusu mpaka ndani ya Ziwa Nyasa. Mgogoro huo ulitaka kufifisha mahusiano mema ya kidiplomasia baina ya Malawi na nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua umuhimu wa mahusiano ya nchi, namwomba Mheshimiwa Waziri alieleze Bunge, mgogoro huu umepatiwa ufumbuzi au bado? Kama bado, Waziri aje hapa atueleze, nini kinaendelea? Je, huo mpaka ndani ya Ziwa Nyasa, nchi yetu ina eneo la ukubwa gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Umoja wa Mataifa (UN) umetutaka mataifa yote yapige vita Mataifa yanayotuhumiwa kuzalisha makombora ya nyuklia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, kuna taarifa zinaeleza kwamba baadhi ya Balozi za nchi yetu huko ng‟ambo zipo taabani kifedha. Namwomba Mheshimiwa Waziri alieleze Bunge hili hali halisi ya kifedha kwa ofisi za Balozi za Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.