Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ni miongoni mwa Wizara zenye umuhimu wa kipekee kwa nchi yetu. Mafanikio ya utendaji kazi wa nchi hii unategemea uwezeshwaji katika rasilimali zote (rasilimali watu na rasilimali fedha). Tabia iliyozoeleka ya Hazina kutoa pesa iliyoidhinishwa na Bunge kwa Wizara zetu ikiwemo hii ya Mambo ya Nje imekuwa kikwazo kikubwa kwa watendaji wa Wizara yetu. Ifike wakati sasa Bunge liheshimiwe kwa kutekeleza maamuzi/maelekezo yake na Wizara zetu zitendewe haki kwa kupewa bajeti walizoidhinishiwa na Bunge lako Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa rasilimali watu yenye sifa stahiki ni muhimu sana kwa utekelezaji wa majukumu ya Wizara hii muhimu, Serikali inabidi iweke mkazo wa kipekee kuandaa Mabalozi wetu wanaotuwakilisha nje ya nchi na watendaji wa Wizara. Lazima foreign service officers wapewe mafunzo maalum ya muda mrefu (angalau mwaka mmoja) ili kupata vyote, Regional and functional specializations kwa watendaji wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Regional specialization ni lazima ijumuishe mafunzo ya lugha kuu ya eneo (region) husika. Kwa mfano, Watendaji wetu kwa Kurugenzi ya Mashariki ya Kati (Middle East and North Africa) ni lazima wawe na umahiri wa lugha ya Kiarabu. Kurugenzi ya Ulaya wajue Kifaransa na Ki-Spanish na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu Wizara hii pia itoe umuhimu wa kipekee kwa Chuo cha Diplomasia ili kiwe na hadhi stahiki. Kwa sasa Chuo kiko katika hali mbaya, miundombinu yake kwa kweli hairidhishi, lakini hata Walimu wa Chuo cha Diplomasia hawapatiwi mafunzo stahiki ya kuwajengea uwezo kwa kuandaa watendaji wa Wizara hii. Kozi fupi nje ya nchi kwa Walimu wa Chuo hiki ni muhimu sana ili kuwajengea uwezo katika kutekeleza majukumu yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika harakati/jitihada za kubadili hali ya Chuo cha Diplomasia iliwahi kuundwa Tume ya Profesa Ishumi iliyojumuisha Wataalam mahiri wakiwemo Profesa Daudi Mukangara. Ni muhimu taarifa ya Tume hii ifanyiwe kazi. Kuwa na Wakuu wa Chuo wenye sifa bila ya kufanyia kazi masuala mengine muhimu haitoshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo muhimu sasa Wizara ibadili utendaji kazi wake na utoaji taarifa zake za kila mwaka ikiwemo Hotuba zake za Bajeti za kila Mwaka. Wizara isitoe descriptive report tu, ni lazima kutoa taarifa zinazoonesha kuwa Wizara ilikuwa na malengo yanayopimika (measurable goals/objective). Hili liwe pia kwa Balozi zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima Balozi zetu zipewe malengo maalum ya kuyafikia na malengo hayo yazingatie maeneo waliko kulingana na maeneo/nchi wanazotarajia kupata wawekezaji, watalii na kadhalika. Kwa mfano, malengo ya Wizara kwa mwaka ujao wa fedha hasa Kifungu cha 193 (i, ii, iii na iv) yangeweza kuboreshwa na kutaja vigezo mahususi.