Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya na fursa ya kuchangia leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri na pia kwa kuteua viongozi wenye uzoefu katika Wizara hii ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na bajeti ndogo katika Wizara hii, tunashauri Serikali ipeleke fedha kwa wakati ili majukumu yatekelezwe vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashauri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ifanye juhudi na kukaa na Wizara zingine (Coordinate) katika kuboresha huduma za Wizara na pia kuongeza fursa ya kiuchumi na kimahusiano ya nchi yetu Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri masuala machache ya kuboresha huduma na fursa kwa Watanzania. Kwanza, naomba Watumishi wetu, Waheshimiwa Mabalozi wetu wapatiwe mafunzo ya kiuchumi na marketing namna ya kuitangaza nchi yetu (economic diplomacy), Mabalozi wa nchi nyingi hufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze wachache niliopata fursa ya kukutana nao mfano, Balozi wetu wa China na Netherland, pia wapate uwezo wa kutafuta masoko ya bidhaa zetu na pia tunapohitaji bidhaa huko watupatie maelezo au vielelezo. Ni muhimu Wizara iwe na dirisha la kuhudumia Watanzania wanaotaka kuagiza bidhaa nje na fursa ya kuwekeza nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Tanzania iangalie namna ya kutumia Watanzania wanaoishi nje na waliokuwa Watanzania na sasa ni raia wa nchi zingine kutokana na mazingira diaspora. Nashauri tuwe na pass au utambulisho maalum ambao utawapa fursa waliokuwa Watanzania na sasa raia wa nchi zingine ili warudi kutembelea nyumbani wapate haki zote sawa na Watanzania isipokuwa kufanya kazi za umma (Serikalini), kuchagua na kuchaguliwa mfano, ni nchi ya India. Tuangalie pia hao raia ambao watoto wao pia wawe na hiyo haki, ambapo leo hawana (Persons with Tanzania Origin).
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, Wizara iboreshe Chuo cha Diplomasia na pia ishirikiane na Wizara ya Elimu kuboresha mitaala na mafunzo ya International Relations. Leo hii wanafunzi wetu wa International Relations hawana viwango kabisa, lugha ni shida, wacha lugha nyingine hata kiingereza ni shida. Vijana wetu wangekuwa wanajua lugha nyingi hata ajira ya ukalimani wangepata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Diplomasia kiongezewe bajeti kuboresha huduma mbalimbali ili wanaotoka au kuhitimu hapa, waweze kupata ajira kokote katika mashirika ya Kimataifa na pia taasisi za ndani na nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, tunashauri pia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki iwatumie Mabalozi wetu kufanya jitihada ya kuunganisha Taasisi za huko waliko ili kuboresha Taasisi zetu. mfano, vyuo kama SUA, Chuo cha Nelson Mandela, vituo vya utafiti mbalimbali, tuwe na Program za kushirikiana (Exchange).
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kutufanyia semina Wabunge wote juu ya masuala ya Itifaki, namna ya sisi kuweza kufanya mawasiliano na viongozi mbalimbali. Suala zima la kuweka heshima yetu na namna ya kutuwezesha kufanya mawasiliano (Etiquette and Diplomacy) (Manners and Presentation).