Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kuchukua nafasi hii kuunga mkono hoja ya Kambi Rasmi ya Upinzani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kutoa ushauri wangu kuhusu mabaki ya mjusi wetu yaliyoko Humberg. Ni aibu kwa Serikali yetu na nchi yetu ya Tanzania kushindwa kuyarudisha mabaki ya mjusi wetu. Hayo mabaki tunaendelea kuwanufaisha Wajerumani na sio Watanzania. Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kuyarudisha mabaki hayo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kuishauri Serikali ifanye jitihada na kila iwezalo kuweza kurudisha mabaki hayo ili yanufaishe Watanzania kwani Watalii watakuwa wanakuja kuangalia mabaki hayo kwa tozo ya kiingilio. Ili Serikali iweze kurudisha heshima yake kwa wananchi wake wa Tanzania ilete mabaki ya mjusi wetu yaweze kunufaisha Watanzania wenyewe na si vinginevyo, ni aibu kwa Serikali!
Mheshimiwa Mwenyekiti, ofisi za Balozi zetu zipo hoi, yaani zina hali mbaya sana. Nilitegemea safari hii Serikali ingeona umuhimu mkubwa sana na kuweza kutenga fedha za kutosha ili kukarabati hizo ofisi ili ziwe kwenye hali nzuri. Ni aibu unapokwenda nchi za nje, ukienda ofisi za Ubalozi wa Tanzania ni aibu kubwa, pia inatia uchungu kwa nchi yetu. Balozi zetu kuwa mfano wa ofisi mbaya kuliko kawaida, yaani kuliko nchi yoyote hapa duniani halafu Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anasema, watafungua Balozi zingine. Je, ni kwa gharama zipi? Kwa nini Serikali isione umuhimu wa kukarabati kwanza Balozi zilizopo halafu ndiyo ione umuhimu wa kufungua hizo ofisi za Balozi zingine?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kuishauri Serikali ifanye jitihada ya kuwa na Ubalozi wa Uingereza hapa nchini kwetu. Kwani mtu ukitaka kuomba viza ya kwenda Uingereza ilikuwa lazima uende Nairobi, Kenya. Sasa hivi ukitaka viza ya Uingereza sio tena Kenya bali inabidi uende South Africa. Kwa nini Serikali isione umuhimu juu ya jambo hili kwani inaleta usumbufu mkubwa sana na kero kwa Watanzania. Natumaini Mheshimiwa Waziri, kati ya majukumu yake yote, aweke kipaumbele kwa Ubalozi wa Uingereza uwepo hapa Tanzania.