Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, uwepo wetu kwenye EAC utakuwa na tija kwa Taifa hili na watu wake ikiwa tutatambua na kuzitumia fursa zilizopo ndani ya umoja huo. Pamoja na Ibara ya 10 ya Itifaki ya Soko la Pamoja kuwahakikishia raia wanachama uhuru wa kupata ajira nchi zote za umoja wa EAC. Serikali itupatie takwimu ya Watanzania wangapi wameajiriwa kwenye ajira rasmi za Serikali katika nchi za Umoja wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imekuwa ni masoko kwa bidhaa zinazotoka kwenye nchi za Kenya na Uganda. Hata kwa bidhaa ambazo tunatengeneza kwa wingi hapa nchini kama vyombo vya plastic, viatu vya plastic na kadhalika bado vinavyotoka nje ni vingi kiasi cha bidhaa za viwanda vyetu kukosa soko ndani ya chini. Serikali ieleze ni kwa namna gani tukalinde viwanda vyetu ndani ya nchi, kuna udhibiti wowote wa uingizaji bidhaa hizi ndani ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na nchi yetu kuwa na vivutio vingi ya utalii bado hatujaweza kuvitangaza kikamilifu ili tuweze kunufaika vizuri. Ni kwa namna gani tunatumia Balozi zetu zilizoko katika maeneo mengi kutangaza utalii na vivutio vyetu huko waliko?
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuwezesha Balozi zetu ni muhimu sana ili ziweze kutekeleza vizuri majukumu yao. Ni aibu kwa Maafisa wa Ubalozi kushindwa kulipia nyumba za kuishi na kubaki wakilalamika mara kwa mara kila tunapokwenda nje. Maofisa hawa wanalalamikia shida, tabu na kutelekezwa na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuelekea kwenye kutumia sarafu moja kwa nchi zote za EAC. Tumejiandaa kiasi gani? Kwa sasa hiyo shilingi ya Tanzania ndio yenye thamani ndogo sana tofauti na fedha za wenzetu. Tusikubali mambo ambayo yatakuja kutuumiza kama hatujajipanga vizuri ndani ya nchi. Tusije tukawa wasindikizaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na nchi yetu kuwa na vyuo vinavyotoa mafunzo ya fani za utalii na customer care; bado mahoteli mengi makubwa na madogo watumishi wengi ni kutoka Kenya na wanatoa huduma nzuri sana na wanaipenda kazi yao. Naomba Serikali itueleze nini kinakosekana ndani ya vyuo vyetu hapa nchini au kwa vijana wetu wanaosoma fani hiyo kiasi cha kutokubalika kwenye hoteli zetu. Je, Serikali imefuatilia mitaala ya vyuo vya utalii vya Kenya na kuona upungufu wetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lipange utaratibu wa Wabunge wa EAC wawe wanatoa semina na mafunzo kwa Wabunge kuhusu yale wanayofanya ndani ya Bunge la EAC ili tupate uelewa mpana na up to date yanayoendelea kuliko kusubiri hotuba wakati wa bajeti ya Serikali.