Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia kwenye hoja hii muhimu, lakini kwa namna ya kipekee naomba nichukue fursa hii kukupongeza sana kwa kazi nzuri unayoifanya ya kuongoza Bunge lako Tukufu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza Waziri na Naibu wake wa Fedha kwa bajeti yao iliyokuwa nzuri. Lakini kwa namna ya kipekee naomba nichukue fursa hii kuipongeza Serikali kwa kuanza kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kutenga asilimia 40 ya bajeti ya mradi wa maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa kuipongeza sana Serikali kwa kuanza kutekeleza ahadi za Mheshimiwa Rais, za kupeleka shilingi milioni 50 kwenye kila kijiji na kwenye Serikali za Mitaa. Naiomba Serikali ihakikishe inatengeneza utaratibu unaoeleweka kusudi zile hela shilingi milioni 50 ziweze kuwafikia walengwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumshauri sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwamba moja ya majukumu ya Bunge ni kuishauri Serikali, lakini leo hii tumeona Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumzia sana tatizo la maji. Nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri, sisi Wabunge tumetumwa maji kwenye maeneo yetu, kwa hiyo tunataka tuone maji yanatoka. Katika eneo hili Wabunge wametoa hadi utaratibu ambao unaweza kutusaidia tukapata hela kwenye maeneo hayo. Kwa hiyo, sioni sababu ya Mheshimiwa Waziri kuanza kusita tumesema tuongeze shilingi 50 kwenye tozo la mafuta kwa maana ya dizeli na petroli. Sisi wenyewe Wabunge ndiyo tutakuwa tuko tayari kwenda kuwasemea wka wananchi kusudi wajue kwa nini tumeongeza pesa hizo, sasa sioni sababu ya Serikali kusita kwenye eneo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, adha ya maji inaeleweka na wanaopata tabu katika eneo hili ni wakina mama na ndoa nyingi zimekuwa zinamashaka kwa sababu ya tatizo la maji katika mjini pamoja na vijijini. Kwa hiyo, namuomba sana kaka yangu Waziri wa Fedha pamoja na Naibu wake waliangalie hili jambo kwamba moja ya miongoni mwa sera za Chama cha Mapinduzi ni kuhakikisha watu wanapata maji katika maeneo yao. Na hapa sisi kama Wabunge tumetoa commitment kwa kusema tuko tayari kuruhusu tutoe shilingi 50 kwenye mafuta ya dizeli na petroli kusudi tuhakikishe wananchi wetu wanapata maji katika maeneo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunamuomba sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri waliangalie hili jambo watakapokuja kuhitimisha hapa waone asilimia karibu 95 au 96 ya Wabunge wote wanataka kuhakikisha maji yanapatikana katika maeneo yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati ya Bajeti wakati inajadiliana na Wizara ilitoa mapendekezo na ilikubaliana na hoja kwamba ile tozo ya shilingi 50 sehemu ya tozo ya shilingi 50 ipelekwe kwenye afya kwa maana ya kuboresha vituo vya afya na zahanati. Kwa hiyo, hatuna sababu ya kutokukwepa kwenye eneo hili. Ni lazima tukubaliane na hii hoja kusudi wananchi walio wengi wapate huduma kwenye afya pamoja na zahanati.
Mheshimiwa Naibu Spika, sababu alizokuwa anazitoa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwenye eneo hili, wanasema kwamba kuongeza tozo kwenye eneo hili tutakuwa tumeongeza mfumko wa bei. Siyo kweli, mwaka 2015 bajeti iliyopita tuliongeza tozo ya shilingi 50 kwenye maeneo haya, wakati uli mafuta yalikuwa yana rank kutoka shilingi 2100 mpaka 2500 na sasa hivi mafuta yana rank toka 1600 mpaka 1900 na mfumko wa bei uliendelea kubaki vilevile. Kwa hiyo, ninataka kumwambia Mheshimiwa Waziri asiingie woga kwenye eneo hili, watu wanataka maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuomba hela hizi za maji naiomba Wizara ihakikishe hizo hela zinaenda kwa wakati kumekuwa kuna tatizo la kuzichelewesha hizi hela ziende kwa wakati kwenye maeneo haya. Matokeo yake ni kusababisha miradi ya maji kuendelea kuwa ya gharama zaidi, kwa sababu mradi unapochelewa kufanyiwa kazi automatical gharama za maji zinapanda.
Leo hii sisi Wabunge wa CCM ndio tupo ndani tunajadili, kwa hiyo tunamwomba sana Waziri wa Fedha akubaliane na hoja hizi kwa sababu ndizo zinazowagusa wananchi waliokuwa wengi. Tutaonekana Wabunge wa CCM tumetoa maamuzi mazuri kwa maslahi ya Taifa hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka kulizungumzia ni suala la kilimo. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, alisema asilimia 67 mpaka 72 ya Watanzania wanategemea kilimo, na yeye mwenyewe, wakati anazungumzia suala la mpango alizungumzia asilimia 67 ya Watanzania wanategemea suala la kilimo. Kulikuwa hakuna sababu ya kutokuongeza ruzuku ya pembejeo katika eneo hili. Kwa hiyo, tunamuomba Waziri aliangalie hili jambo.
Mheshimiwa Naibu Spika, yeye mwenyewe Mheshimiwa Waziri amekuja hapa ametuambia tuna kwenda kwenye mpango wa Viwanda, tunaendaje kwenye mpango wa viwanda kama malighafi hatuwezi kupata kutoka kwenye kilimo? Tunamwomba Waziri kusudi tuweze kupata malighafi ya kutosha, lazima tuhakikishe wakulima wanapata pembejeo kwa bei rahisi na wamesaidiwa katika eneo hili. Kwa hiyo, nataka nimuombe ndugu yangu aliangalie na hili jambo la kuongeza mfuko wa pembejeo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala la Benki ya Kilimo, hili ni suala very sensitive na ni nyeti sana, kwa hiyo tunaomba kwenye benki hii waongezewe mtaji, na ifunguliwe matawi yote katika nchi hii ya Tanzania kusudi wale amabo tumewakusudia waweze kusaidiwa katika maeneo husika. Tuna kwenda kwenye uchumi wa viwanda, lengo kubwa ni kuhakikisha tunapata mapato ya kueleweka na tunapata ajira. Serikali inajitahidi kuwashauri wawekezaji wa ndani na nje kwenye eneo hili waje kuwekeza. Na wawekezaji wanawekeza kwa nguvu kubwa sana, itakuwa ni kosa kuendelea kuzitoza malighafi katika eneo hili. Kwa hiyo, nilikuwa namuomba Waziri anapokuja atuambie kwa nini ameamua kutoa tozo ya crude oil kutoka sifuri kwenda asilimia kumi. Tayari watu wameshawekeza hela zao pale na tayari kuna ajira ya uhakika katika eneo hili. Ni vyema aangalie ni utaratibu gani utakaotusaidia kupata kodi, kwenye eneo la wafanyakazi Pay As You Earn na kwenye kodi za kawaida. (Makofi)
Eneo lingine ambalo nataka kulizungumzia ni eneo la utalii. Katika bajeti iliyopita utalii ulichangia asilimia 17 kwenye Pato la Taifa na ilikuwa utalii inaongoza kwenye kuchangia katika Pato la Taifa lakini leo hii tunaweka...
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.