Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuunga mkono hoja. Nampongeza Mheshimiwa Waziri Mahiga, Naibu wake na timu nzima ya Wasaidizi wao katika Wizara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuchangia hoja kwa kuelezea masikitiko yangu ya utoaji wa Visa katika Balozi zetu zilizopo katika nchi mbalimbali. Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia tunataraji Serikali sasa imefika wakati tuanzishe utaratibu wa kutoa Visa online, utaratibu huu sasa wa watu kutakiwa waende wenyewe moja kwa moja ni wenye usumbufu na umepitwa na wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni Wizara ione umuhimu pia wa kufungua ofisi za ubalozi wa Tanzania Korea ya Kusini, kule kuna potential kubwa ya kunufaika na fursa za teknolojia na watalii kutembelea nchi yetu. Pia Balozi zetu kutumika vizuri kwa kutangaza Tanzania kiutalii na fursa nyingine za kibiashara ili nchi yetu inufaike na uwepo wa Balozi hizo badala ya utaratibu wa sasa wa kutoa Visa tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara pia ione umuhimu wa kuongeza kasi ya kujenga au kununua majengo kwa ajili ya Balozi zetu wenyewe, baada ya miaka 55 ya uhuru badala ya kuendelea kupanga wakati nchi nyingine ndogo kama Eritrea zimejenga nyumba zao wenyewe. Umefika wakati sasa Serikali iongeze kasi ya ujenzi au ununuzi wa majengo yetu wenyewe kwenye Balozi hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante.