Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri. Niiombe Serikali yangu ijipange katika suala zima la wafanyabiashara kwani hawa wanaongeza pato kubwa katika Taifa letu, lakini kunakuwa na ukiritimba wa passport pamoja na Visa. Sambamba na hayo VAT inakuwa ni shida kwa wafanyabiashara hawa, yaani mzigo unachajiwa mara mbili ya bei aliyonunulia mfanyabiashara huyu. Suala la utoaji wa passport unachukua muda mrefu kuipata kwa hiyo niishauri Serikali yangu iliangalie hili pass hizo zitoke kwa muda muafaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la Mabalozi wetu hawa imefikia wakati sasa watafute wawekezaji pamoja na wafadhili kwa ajili ya kujenga nchi yetu sasa kiuchumi zaidi.
Katika Jimbo la Lushoto kuna ma-sister wana miaka zaidi ya 60 na wamesaidia sana jamii inayowazunguka na mpaka sasa wanaendelea kusaidia. Wamejenga shule, wamejenga zahanati na wamejenga hosteli na pia wanajitolea kuwafundisha watoto wa maeneo hayo. Kwa kuwa ma-sister hawa ni wa muda mrefu sana na wanaendelea kulipia kodi kama kawaida, lakini kwa sasa hawa wamezeeka na shirika limefika hatua wanashindwa kuwalipia ma-sister wale. Niiombe Serikali yangu iweze kuwapa uraia kwani wakiondoka na kurudi kwao itakuwa ni hasara kubwa sana kwa wananchi wa eneo lile la Kifungilo sekondari pamoja na Kata ya Gare kwa ujumla itakosa huduma muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba Mheshimiwa Waziri atembelee Jimbo la Lushoto au atume Mjumbe ili akaone hali halisi kwa haya niliyoongea hasa kwa suala zima la misaada tunayopatiwa na ma-sister hawa, kwa maelezo zaidi Mheshimiwa Waziri naomba nimwone ili nimwelezee kwa undani zaidi.