Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Balozi zetu katika nchi mbalimbali hali siyo nzuri sana, Serikali iboreshe ukarabati wa majengo katika Balozi zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mabalozi waliostaafu bado wako nchi za nje, nashauri walipwe haki zao na kurudishwa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabalozi waitangaze nchi yetu kibiashara katika nchi mbalimbali kwa mfano watangaze Mlima Kilimanjaro kuwa upo Tanzania na siyo Kenya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabalozi wawe na wataalam ambao wanaweza kufanya research katika nchi wanazowakilisha ili kupata mahusiano mazuri ya kibiashara na pia kupata ajira kwa vijana wetu katika nchi mbalimbali. Pia Serikali iwape fedha Mabalozi wetu kwa muda muafaka siyo kuchelewesha malipo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.