Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Pia nimpongeze Mheshimiwa Balozi Mahiga, Naibu Waziri wake pamoja na Watendaji wake kwa kazi nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina masuala kadhaa pamoja na kuunga mkono hoja, nitaomba yajibiwe au kama bado yafanyiwe kazi na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, diplomasia imejikita katika misingi ya reciprocity. Tupewe ufafanuzi kama kweli Balozi wa nchi za nje hawataruhusiwa tena kwenda mikoani bila kibali cha Wizara ya Mambo ya Nje. Naamini jambo hili haliwezi kuwa kweli, hii maana yake watu hawatakuwa na uhuru kamili kufanya kazi zao halali nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakiamua ku-retaliate na kuweka sharti hili kwa Mabalozi wetu walio nchi zao inaweza kutuumiza. Nitaelewa kama kwa sababu ya usalama Mabalozi na Maofisa wao watatakiwa kutoa taarifa ya safari zao nje ya Dar es Salaam ili Serikali ikibidi iwawekee ulinzi, hiyo inaeleweka, lakini hivi sasa ni kama suala hili limepotoshwa na Wapinzani kudai wanahitaji ruhusa. Mheshimiwa Waziri atufafanulie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Balozi zetu ziruhusiwe kubaki na maduhuli wanayoyakusanya ili kupata fedha za kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jumuiya ya Afrika Mashariki imeendelea kutoeleweka vizuri kwa wananchi, ingekuwa vizuri kupata kitabu cha maswali na majibu (Q and A) kuhusu maana ya ushirikiano – sekta kwa sekta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka ya nchi hii yote bado haijakamilika. Mpaka kati ya Uganda na Tanzania huko Kagera, uliowahi kusababisha vita hadi leo haujakamilika. Mheshimiwa Waziri wa Ardhi atueleze ni lini wanakamilisha zoezi hilo. Nilijaribu kulikamilisha nilipokuwa Waziri wa Ardhi, lakini jukumu la mwisho ni Waziri wa Mambo ya Nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alikuwa Mwenyekiti wa Governing Council ya UN–Habitant kati ya 2006 – 2008. Katika wadhifa huo alikuwa Co–Chair wa World Urban Forum ya Vancouver Canada 2006. Kwa kuwa, mkutano wa Habitant III, utafanyika Oktoba Ecuador ni mkutano unaotokea kila baada ya miaka 20. Mheshimiwa Waziri unashauriwa ku-check kuona kama Rais anaweza kuhudhuria mkutano huo. Kwa hivi sasa Mheshimiwa Rais wetu tayari anasifika duniani, akihudhuria Habitant III jambo hilo Kidiplomasia litaendelea kumsimika kama “Purposeful Traveller”.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni maoni yangu kama yakionekana yanafaa yafanyiwe kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.