Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na timu nzima ya Wizara kwa hotuba nzuri ya bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia ya leo uhusiano wa Mataifa ni sehemu ya kukuza uchumi na pia ni kipimo cha Nation Brand. Tanzania ina sifa kubwa na heshima kwa nchi nyingi duniani kutokana na utamaduni, amani, demokrasia na hata historia ya kuwa mstari wa mbele katika ukombozi wa Afrika. Economic diplomacy inaenda pamoja na branding ya nchi yetu kwa kuhakikisha tunaimarisha Nation Brand ya Tanzania. Hii ni pamoja na kuhakikisha Balozi zetu zinaendelea kuitangaza Tanzania na kuangalia ni jinsi gani nchi yetu inakuwa na competitive advantage na nchi jirani na Bara zima la Afrika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza Wizara iendelee kuangalia namna ya kuimarisha diaspora katika kuchangia uchumi wa Tanzania. Nchi zinazoendelea zilizo nyingi zinategemea sana fedha ya kigeni kutokana na diaspora. Tunapoangalia ushiriki wa diaspora katika uchumi wetu, napendekeza Wizara iweke utaratibu wa vijana wetu kupanua ajira ya nchi za nje. Kutokana na changamoto za ajira ni bora pia kuangalia soko la ajira la nchi za nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na maneno ya mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi. Napendekeza Mheshimiwa Waziri aliambie Bunge huu mgogoro wa mpaka kama upo umefikia wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu sasa nchi jirani imetumia fursa tulizonazo hapa nchini kuzitangaza kuwa zipo kwao. Napendekeza Wizara ichukue hatua mahsusi kukomesha tabia hii. Pia ni wakati muafaka kwa Wizara kuangalia fursa za kibiashara hasa kwa nchi mpya kama Sudan ya Kusini.