Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema na kuniwezesha kuchangia hotuba hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kuhusu deni la matibabu ya ndugu yetu, Marehemu Nassor Moyo ambalo hadi leo Serikali ya Uingereza inadai Tanzania. Deni hili ni aibu kubwa kwa nchi yetu, ni vyema Mheshimiwa Waziri alipatie ufumbuzi suala hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabalozi wetu walioko nje ya nchi wanadharauliwa kwa sababu nyumba wanazoishi haziridhishi na hazina ubora, hii ni dharau. Mabalozi wanaoishi katika nchi yetu ya Tanzania wanaishi nyumba za hadhi na ubora wa hali ya juu. Tunamwomba Mheshimiwa Waziri suala hili alisimamie kwa nguvu zake zote ili lirekebishwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Watanzania walioko nchi za nje wanapopatwa na matatizo au dharura, ni njia gani za mawasiliano watumie kupata msaada wa Kibalozi? Naomba Mheshimiwa Waziri atufafanulie suala hili.