Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naanza kuchangia hotuba hii kwa kumshukuru Mungu kwa kunijalia kuwa miongoni mwa Wabunge wa Bunge hili. Pili nachukua fursa hii kumpongeza Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuonesha imani na uwezo mkubwa wa kuongoza nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, nawapongeza wapiga kura wangu kwa kunichagua kwa kura nyingi kuwa Mbunge wao. Natambua imani yao kubwa waliyonayo kwangu na nawaahidi sitowaangusha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia hotuba hii napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, sifa na muda wa wafanyakazi wa Ubalozini. Napenda kuipongeza Wizara na Serikali kwa jumla kwa utaratibu mzuri wa kuwapangia na kuwateua wafanyakazi wa Balozi zetu. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni sifa gani wanazotumia katika kuwateua wafanyakazi wetu pamoja na Mabalozi katika nchi za nje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Diplomasia. Nachukua nafasi hii kuipongeza Wizara kwa kukiendeleza chuo hiki muhimu katika kuzalisha na kutayarisha wataalam wetu. Chuo hiki kama vilivyo vyuo vingine kinahitaji mahitaji kama vile mikopo na kadhalika. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri kuna mpango gani wa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma katika chuo hiki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Jumuiya hii ni ya muda mrefu na ina uzoefu mkubwa. Napenda kueleza wasiwasi wangu juu ya ongezeko la nchi wanachama wa jumuiya hii. Nchi hizi zilizo nje ya Afrika Mashariki zina matatizo makubwa katika nchi zao na ndiyo wanaotuongezea watu katika mipaka yetu. Aidha, zimetuongezea uhalifu na ujangili na matatizo mengine. Hivyo, namwomba Mheshimiwa Waziri aliangalie suala hili na wasite kuongeza wanachama walioko nje ya Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.