Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Buyungu, Wilaya ya Kakonko bado kuna migogoro midogo midogo ya wananchi wanaoingia Burundi na Warundi wanaoingia Tanzania, wanapata usumbufu wa hapa na pale hasa ule wa polisi. Wilaya imepakana na Burundi kwa eneo lote la Magharibi yaani Vijiji vya Mugunzu/Kiduduye, Katanga, Ihabiro, Gwanumpu, Bukirilo, Malenga/Kikulezo, Kiga, Kasuga, Nyakeyenzi, Muhange, Gwarama/Kabare, Nyakibuye, Rumeshi, Kinyinya na Nyanzige (Kata ya Nyamtukiza).
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakazi hawa wanapata usumbufu kwenda kuuza au kununua mazao/biashara Burundi. Wananchi hawa wanakamatwa na polisi na kunyanga‟anywa bidhaa na fedha bila sababu. Aidha, Warundi nao wananyanyaswa na polisi na kuibiwa/kunyang‟anywa pesa/bidhaa wanazouza au kununua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri yafuatayo:-
(i) Umoja wetu wa Afrika Mashariki uwanufaishe wadau wa nchi
wanachama;
(ii) Polisi wazuiliwe kuwaonea na kuwanyang‟anya Warundi bidhaa toka Burundi mfano kama bia za Primus, Amstel, sabuni na kadhalika; na
(iii) Masoko ya mipakani (Burundi/Tanzania) yasiwekewe vikwazo vya nani/nini uuze/ununue kutoka nchi zetu za Burundi na Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitaifa nina ushauri ufuatao:-
(i) Viza za nchi zote zenye Mabalozi hapa nchini zitolewe humu nchini bila urasimu kama za Uingereza zinatolewa South Africa;
(ii) Mabalozi/ofisi za Tanzania nje ya nchi watangaze vivutio vya utalii vilivyopo hapa nchini kama vile hoteli za kitalii, mbuga za wanyama, Mlima Kilimanjaro na kadhalika. Mfano miaka ya 2005-2008 Uingereza hapakuwa na matangazo ya kutosha kwa watalii kuja Tanzania na hata hoteli zilizoonekana ni za Kenya na Zanzibar tu. Mlima Kilimanjaro uliendelea kujulikana kama upo nchi ya Kenya; na
(iii) Afrika Mashariki haijatulia hasa viongozi wa nchi pale wanapogombania rasilimali zinazopatikana nchi moja au nyingine. Kwa mfano mafuta ya Uganda kuletwa Tanzania, Kenya haifurahi, reli kwenda Rwanda toka Tanzania baadhi ya nchi wanachama hawafurahii. Nashauri wakae na kuelewana ili chokochoko ziishe.