Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi kwa dakika tano nizungumze kuhusu Wizara muhimu sana, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ambayo inahusiana na ushirikiano wa nchi mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama walivyozungumza wenzangu kuhusu Ubalozi wetu mdogo pale Lubumbashi, madereva na wafanyabiashara wetu wanapata tabu sana pale. Ubalozi mdogo Lubumbashi ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uchumi wa nchi yetu Congo ni muhimu sana kuliko Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi. Kwa hiyo, ni muhimu sana kuikamata Congo kwa sababu ni nchi kubwa, ina watu wengi na ina kila kitu itasaidia sana uchumi wa nchi yetu na tukiimarisha reli ya kati. Niliomba siku nyingi na nilipokuwa Kamati ya PAC tuliomba Ubalozi mdogo Lubumbashi na kama haiwezekani tumtafute Mtanzania yeyote ambaye yupo pale apewe hadhi ya kibalozi kusaidia wananchi wetu wale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu Muungano. Yupo Mbunge anazungumzia mambo ya ajabu kabisa kwamba tumewapunja, sheria ya masuala haya ya mambo ya nje lazima Waziri mmoja atoke Zanzibar sijui Waziri wa Mambo ya Ndani atoke Zanzibar. Ndugu zangu tuna Mawaziri watatu muhimu, Waziri wa Ulinzi katoka Zanzibar, Mheshimiwa Dkt. Mwinyi, tuna Wizara kubwa ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano chini ya Mheshimiwa Profesa Mbarawa, Naibu Waziri yupo hapa Mheshimiwa Masauni bado mnataka nini zaidi? Ndugu zangu tukitaka hivyo hata sisi tutasema, kwa mujibu wa population ni four percent. Hata mimi Rukwa nitasema tunataka Waziri maana hatuna Waziri na tuna idadi ya watu kama Zanzibar mbona hatuna Waziri hata Naibu Waziri na hatulalamiki hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unakuja kulalamika hata Rais akitaka kwenda nje awachukue Wazanzibari. Rais Magufuli anasema safari za nje hakuna unakuja Bungeni unataka safari za nje, hakuna tegemea pesa zako uende nje. Tusianze kuleta mambo ambayo hayatakiwi kwenye Muungano, tumeshaungana ndiyo hivyo hivyo, sasa ninyi mnataka nusu kwa nusu ndugu zangu? Itawezekana wapi? Haiwezekani ndugu yangu! Nusu kwa nusu haiwezekani! Ninyi mpo four percent mtapata four percent ya kila kitu.
Mheshimiwa Khatib tulia, usipige kelele hapa kwamba mnataka Mabalozi wengi, hapana! Nchi yote tuna Mabalozi 21 mkipata hata Naibu Mabalozi shukuru Mungu. Mheshimiwa Khatib tukikuambia ulipie Balozi mmoja tu nchi yako italipa gharama ya Balozi kule nje?
Mheshimiwa Khatib tulia, usipige kelele hapa kwamba mnataka Mabalozi wengi, hapana! Nchi yote tuna Mabalozi 21 mkipata hata Naibu Mabalozi shukuru Mungu. Mheshimiwa Khatib tukikuambia ulipie Balozi mmoja tu nchi yako italipa gharama ya Balozi kule nje?
Tulieni! Hatuwezi kwenda hivyo unasimama hapa unasema sisi tumepunjwa, hamkupunjwa kitu bado tumewasaidia. Bungeni hapa mmekuja 54, mngejaa kule Zanzibar mngeenea kwenye Jimbo ninyi Ma-CUF, mngeweza kuenea kule kweli? Tukiwaambia tu sasa hivi nendeni kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine amezungumzia ndugu yangu, mimi nilikuwa kwenye Kamati ya PAC kuhusu mgonjwa kutoka Zanzibar, mgonjwa yule alipelekwa na Serikali ya Zanzibar hakuna kukanusha hapa. Nilikuwa mjumbe wa Public Accounts Committee, mgonjwa yule alipelekwa na Serikali ya Zanzibar na atahudumiwa na Serikali ya Zanzibar, Serikali ya Tanganyika ilisema ahudumiwe kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafahamu kwa sababu nilikuwa mjumbe wa Public Accounts Committee hesabu hizi zilikuja kwetu. Huyu bwana alipelekwa na Serikali ya Zanzibar akatibiwe kule, Wizara ya Afya siyo ya Muungano. Kwa hiyo, hili deni ni la Serikali ya Zanzibar likadaiwe huko huko, hatuwezi kulipa sisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ndugu zangu tusiende papara kwa habari za kutaka zaidi vyeo au namna gani na sisi tutadai vyeo. Rais anapanga Mawaziri kutokana na jinsi anavyotaka yeye huwezi kumlazimisha awape Zanzibar Mawaziri 10 au 15, ninyi kwanza kule kwenu mna Mawaziri zaidi ya 20, mna Wabunge kule kwenu hawatoshi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine na nimezungumza mara nyingi hapa, Wizara ambazo siyo za Muungano muwe mnatungoja nje tunabaki peke yetu hapa tukimaliza za Muungano ndiyo tunawaita mnaingia ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani uje kuchangia Wizara ya Kilimo inakuhusu? Wizara ya Maji inakuhusu. Kwa hiyo, muwe mnachagua Wizara za kuchangia kuanzia sasa, changia Wizara inayokuhusu basi Wizara nyingine tuachiaeni wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.